• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wilaya ya Mkalama yaungana na Watanzania wote kuadhimisha miaka 58 ya Muungano wa Tanzania

Imewekwa kwenye: April 26th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Mfaume kizigo amesema kuwa katika kuazimisha miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Tanzania  imefanikiwa pakubwa kutatua kero za Muungano ikiwa ni pamoja na kuimarisha umoja na mshikamano na kuimarisha ulinzi na usalama kwa Nchi.


Ameyasema hayo wakati akihutubia Katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Muungano yaliyofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambapo ametaja mafanikio hayo yanatokana na misingi mizuri na Muunganiko walioufanya waasisi wa Taifa hili Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.


"Asili yetu, Babu zetu ni wamoja sisi sote tumeingiliana kidamu, hauwezi kuchagua ndugu ukishazaliwa naye  ndugu ni ndugu hata kama haumtaki, undugu wetu ni wadamu na tunapendana hadi Leo Nchi yetu inaadhimisha miaka 58 ya Muungano tumepitia mambo mengi kero za Muungano zimepungua sana sana, tumepiga hatua kubwa ya maendeleo kiuchumi, ulinzi, kiusalama  , kijamii na hata kisiasa".Aliongeza Dc Kizigo.


Pamoja na hayo amesema kuwa Matunda ya Muungano yanaonekana Kwa Nchi hivyo kuwataka wananchi kuendelea kuyaenzi Kwa kufanya kazi kwa bidii , kuendelea kudumisha amani na utulivu ,kuendelea kufuata Sheria za Nchi pamoja na kuendeleza uzalendo ambao uliachwa na waasisi wa Tanzania Kwa kuwa tayari kujitoa kwaajili ya Nchi yao.


Pamoja na hayo aliwataka wananchi kujiandaa na maandalizi ya sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 23 Mwaka huu kwakuwapa ushirikiano wataalamu watakaopita kwenye Kaya zao kwakutoa  taarifa muhimu kwani kwakufanya kivyo inapelekea Serikali kuweza kupanga bajeti  na kuboresha huduma kwa jamii kwakuainisha vipaumbele mbalimbali kulingana na uhitaji wa jamii.


Awali akiongea katika hafla hiyo Afisa Mazingira Wilaya ya Mkalama Bw.  Amon Sanga amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama imeungana na watanzania wote kuadhimisha siku hii muhimu Kwa kufanya usafi katika eneo la Halmashauri pamoja na kupanda miti mbalimbali ikiwa  ni kuunga mkono juhudi za waasisi hao na kuhakikisha mazingira yanaendelea kutunzwa na kuboreshwa.


Baadhi ya wananchi walihudhuria katika hafla hiyo wameeleza namna wanavyouenzi Muungano kwakufanya kazi kwa bidii Ili kuendelea kupinga Adui wa  Maendeleo ambayo  ni  ujinga , Maradhi na umasikini na kuongeza kuwa Ili kuweza kupambana na hayo yote lazima umoja uwepo baina ya Tanzania bara na Visiwani ili kwapamoja kuweza kuingiliana na kuishi pamoja.


"Mtanzania anayetoka bara akifika Zanzibar ajisikie yupo Tanzania na walio Zanzibar wakifika Tanzania bara wajisikie wapo Tanzania".

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.