• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MKALAMA WATOA ELIMU KWA WANAFUNZI WA KIKE KUHUSU AFYA YA UZAZI NA HAKI ZAO

Imewekwa kwenye: October 13th, 2025

Katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Kike Duniani, Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wameendesha mafunzo kwa wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Mkalama One, yakilenga kuimarisha uelewa kuhusu afya ya uzazi, usafi wa mwili, haki za mtoto wa kike, na kujitambua.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Mkalama, Bi. Experancia Ngelima, aliwasisitiza wanafunzi hao umuhimu wa kutoa taarifa mara wanapofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia, iwe shuleni au majumbani.

“Kuna mabinti wanafanyiwa vitu lakini hawasemi. Wengine wanatishiwa, wananyamaza. Tukumbuke, mwisho wa siku ni maisha yako. Ukinyamaza, unaweza kuathirika kisaikolojia na kupata msongo wa mawazo. Ukiwa na jambo, tafuta mtu wa kuzungumza naye,” alisema Bi. Ngelima.

Aidha, Bi. Ngelima aliwakumbusha wanafunzi hao kudumisha usafi wa mwili na mazingira, akibainisha kuwa hatua hiyo husaidia kujikinga na magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na uchafu na ukosefu wa huduma bora za usafi hasa kwa wasichana balehe.

Kwa upande wake, Afisa Mwandikishaji wa Mfuko wa Afya Ulioboreshwa (CHF), Bwana Gaffer Venance Mathiacy, alitoa elimu kuhusu manufaa ya kujiunga na mifuko ya bima ya afya ya CHF na NHIF, akieleza namna wanafunzi na familia zao wanavyoweza kunufaika na vifurushi vya huduma za afya vinavyotolewa kupitia mifuko hiyo.

Tukio hilo ni sehemu ya jitihada za Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama katika kuendelea kuhamasisha uelewa wa jamii kuhusu haki, afya, na ustawi wa mtoto wa kike, sambamba na utekelezaji wa sera za serikali katika kulinda na kuinua hadhi ya mtoto wa kike nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MKALAMA WATOA ELIMU KWA WANAFUNZI WA KIKE KUHUSU AFYA YA UZAZI NA HAKI ZAO

    October 13, 2025
  • MGANGA MKUU WA MKOA WA SINGIDA (RMO) ATEMBELEA HOSPITALI YA WILAYA YA MKALAMA KUKAGUA ZOEZI LA MADAKTARI BINGWA

    October 06, 2025
  • MKURUGENZI MKALAMA AWASHAURI VIJANA KUTUMIA MKOPO VIZURI

    September 25, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA LISHE ROBO YA NNE – WILAYA YA MKALAMA 2025

    September 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.