• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI MKALAMA AWASHAURI VIJANA KUTUMIA MKOPO VIZURI

Imewekwa kwenye: September 25th, 2025


Mkalama

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Bi. Asia Messos, amewataka vijana waendesha bodaboda wilayani humo kuhakikisha wanatumia vyema mikopo wanayopewa na Halmashauri kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi na kukuza kipato cha familia zao.


Akizungumza Septemba 24, 2025, wakati wa ziara ya kikazi katika Kijiji cha Nduguti, Kata ya Nduguti, Bi. Messos alikutana na kikundi cha vijana cha Mkombozi, ambacho ni miongoni mwa wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa makundi maalum.


Katika ziara hiyo, Mkurugenzi huyo alitembelea ofisi za kikundi hicho na kukagua shughuli zao za usafirishaji abiria kwa kutumia pikipiki walizonunua kupitia mkopo wa takribani shilingi milioni 25 waliopatiwa na Halmashauri.


“Niwapongeze kwa hatua yenu ya kuungana na kuanzisha kikundi hiki cha ujasiriamali. Naomba sasa mfikirie kufanya makubwa zaidi. Mkirejesha vizuri mkopo huu, Halmashauri ipo tayari kuwapatia hata bajaji,” alisema Bi. Messos.


Aidha, aliwataka vijana hao kuwa mabalozi wa kuhamasisha vijana wengine kujiunga kwenye vikundi vya ujasiriamali ili nao wanufaike na fursa zinazotolewa na serikali kupitia mifumo ya mikopo isiyo na riba.


Bi. Messos alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha maisha ya wananchi kwa kuweka mifumo shirikishi ya kuwawezesha kiuchumi wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia mikopo ya Halmashauri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DAS SULLE AWATAKA WAKULIMA KULIMA KISASA KWA KUFUATA MAELEKEZO YA WATALAAMU

    November 18, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MKALAMA WATOA ELIMU KWA WANAFUNZI WA KIKE KUHUSU AFYA YA UZAZI NA HAKI ZAO

    October 13, 2025
  • MGANGA MKUU WA MKOA WA SINGIDA (RMO) ATEMBELEA HOSPITALI YA WILAYA YA MKALAMA KUKAGUA ZOEZI LA MADAKTARI BINGWA

    October 06, 2025
  • MKURUGENZI MKALAMA AWASHAURI VIJANA KUTUMIA MKOPO VIZURI

    September 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.