• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Watendaji wa Kata na wahudumu wa Afya wahamasishe wananchi umuhimu wa chanjo ya UVIKO 19

Imewekwa kwenye: November 22nd, 2021

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe .Sophia Kizigo amewataka watendaji wa kata na wahudumu wa afya kuongeza kasi ya uhamasishaji  kwa jamii ili wajitokeze kwa wingi  kupata  chanjo ya UVIKO 19 ya awamu ya  pili ijulikanayo kwa jina la SINOPHARM baada ya kufanikiwa kumaliza ya awamu ya kwanza iliyojulikana kwa jina la JANSON JANSON.


Amesama hayo mapema leo wakati akifungua kikao cha Uhabarisho wa  chanjo ya UVIKO 19 kilichojumuisha Wakuu wa Idara na Vitengo watendaji wa Kata na wahudumu wa Afya kilichofanyika katika ukumbi wa Sheketela uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.


Aidha Mhe.Kizigo amewataka watendaji ngazi ya Kata,Wahudumu wa Afya ,wakuu wa Idara na Vitengo kwa umoja wao kuhakikisha wanatoa elimu kwa Wananchi juu ya umuhimu wa kupata chanjo ya UVIKO 19  kwani ni salama na imethibitishwa na Wizara ya Afya.


‘’Tulifanya kikao mara ya kwanza na Viongozi wa wilaya kuhusu uhamasishaji wa Chanjo ya UVIKO 19  ambapo mwanzo tulikuwa na JANSON JANSON, kama wilaya tulifanya vizuri kwa kumaliza chanjo  tulizopewa ,baada ya kikao hicho tuliona ipo haja ya kukaa na watendaji wa kata  na wahudumu wa afya ngazi ya kata ili  kuongeza nguvu ya uhamasishaji.’’ Alisema Mhe.Kizigo Dc Mkalama.


‘’Sasa tumeletewa chanjo  aina ya SINOPHARM dozi 4200 hizi zitatolewa mara mbili tofauti na JANSON JANSON iliyokuwa inatolewa mara moja , tukatoe elimu kwa Wananchi kuwa ni Muhimu mtu akipata chanjo atatakiwa kukaa siku 28 ndipo arudi kuchoma nyingine,hivyo ninategemea baada ya kikao hiki kila mtu kwa nafasi yake atakuwa mwalimu mzuri kutoa elimu juu ya ubora na umuhimu wa chanjo hii ni matumaini yangu hamtaniangusha.’’Aliongeza Mhe.Kizigo .


Naye mratibu wa chanjo wilaya ya Mkalama Duncan Kifaruka amesisitiza ushirikiano baina ya jamii na wataalamu ili kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa kwa kuongeza uwezo wa kutoa huduma kwa sehemu ngumu kufikika ,umuhimu wa ufuatiliaji wa dozi ya pili huku elimu na ushawishi ukiendelea kutolewa kwa jamii  ili chanjo ya UVIKO 19 ikubalike tofauti na kipindi cha mwanzo ambapo chanjo hiyo ilichukuliwa kwa Mtazamo hasi.


Afisa Lishe wilaya ya Mkalama Bi.Eliwandisha Kinyau amesisitiza lishe bora na ulaji unaoshauriwa katika kukabiliana na ugonjwa wa UVIKO 19 ambapo ameshauri ulaji unaozingatia makundi matano ya chakula kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya mwili katika kuimarisha mfumo wa kinga ya  mwili kwani magonjwa ya kuambukiza ikiwemo UVIKO 19  hubadili ufanyanji kazi wa mifumo mbalimbali ya mwili ikiwemo mfumo wa chakula.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.