• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

VISHIKWAMBI 706 KULETA MAPINDUZI YA KIDIGITALI KATIKA SEKTA YA ELIMU

Imewekwa kwenye: January 11th, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhe. Sophia Kizigo leo January 11, 2023 amekabidhi vishikwambi 706 kwa Maafisa Elimu, Walimu  wa Shule za Sekondari na Msingi ili kurahisisha majukumu yao  na kuleta mapinduzi chanya katika Sekta ya Elimu pamoja na kupandisha ufaulu kwa wanafunzi.


Akiongea mapema leo katika makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Sheketela uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. Kizigo aliwataka kuvitunza na kutumia vishikwambi hivyo katika kupata maarifa mbalimbali ya kielimu na kuwa wabunifu katika kuongeza ufaulu Wilayani.


‘’Walimu hamjawahi kuniangusha leo hii mmepokea vishikwambi hivi nendeni mkavitumie kujitajirisha nyie katika masuala ya Elimu na msiende kupiga picha za wanafunzi na kuwaposti Instagram na sehemu nyingine hiyo itakuwa kinyume na sheria na hatua kali zitachukuliwa dhidi yenu" Aliongeza Mhe. Kizigo


Sambamba na zoezi la ugawaji wa Vishkwambi Mhe. Kizigo aliwataka Walimu kuendelea kutekeleza majukumu yao ya kila siku pamoja na kuwahamasisha Wazazi kuendelea kupeleka wanafunzi kuripoti shule kwani tayari masomo yamekwishaanza.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe.James Mkwega  amewasisitiza Walimu kutunza Vishikwambi ili viweze kudumu kwa muda mrefu kwani ni moja ya njia ya mapinduzi ya kidigitali katika Sekta ya Elimu.


Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Bi. Asia Messos aliishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuleta Vishikwambi ambayo ni ahadi ya Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kugawa Vishikwambi katika Wilaya zote nchini ili kutoa motisha kwa Walimu katika kutekeleza majukumu yao. Pia alisisitiza kuwa Vishikwambi ni mali ya Serikali na taratibu zote za uwekaji wa kumbukumbu wa vifaa vya Serikali umefuatwa na zoezi hili la ugawaji linatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 15/01/2023.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.