• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Vijana wahakikishe wanajiandaa kikamilifu kuingia katika soko la ajira

Imewekwa kwenye: March 25th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo amewataka watahiniwa wa kidato cha Sita kujiandaa kikamilifu kuingia kwenye soko la ajira lenye ushindani Mkubwa kutokana na kukua Kwa Sayansi na Teknolojia Duniani.

Ameyasema hayo wakati wa hotuba yake kwenye mahafali ya tano ya kidato Cha Sita ya Shule ya Sekondari  Iguguno iliyopo wilayani Mkalama Mkoani Singida ambapo alisema kuwa ni muhimu wanafunzi kujifunza mambo mengi kama elimu ya uongozi kwani itawasaidia kufanya kazi popote, kuwa na uwezo wa kuwasiliana kwakutumia lugha za picha kuwa na uwezo wa kusikiliza kitu kitakachopelekea kutoa huduma zilizo bora kwa jamii.

Mhe. Kizigo Aliongeza kuwa ulimwengu wa Sasa ni waushindani Mkubwa tofauti na awali hivyo kuwataka kutumia elimu waliyoipata kujua mambo mengi ya kidigitali ( Digital Market) Ili kuweza kupokea fursa zinazokuja kutokana na fani walizosomea pia kufanya mambo mengine ikiwemo kufanya biashara mtandaoni pamoja nakutafuta wateja wapya mtandaoni.

Pamoja na hayo alitumia fursa hiyo kuwapongeza wanafunzi, wazazi pamoja na Walimu kwakushirikiana  kuongeza ufaulu shuleni hapo ambapo Aliongeza kuwa Ili ufaulu uongezeke ni muhimu mafiga hayo matatu yashirikiane huku akiwataka wanafunzi hao kutumia vizuri muda uliobaki kujiandaa na mitihani ya kuhitimu kidato cha sita inayotarajiwa kuanza mapema mwezi Mei.

Awali akisoma risala Kwa Mgeni rasmi Mwl Stephano Mafole alisema kuwa Mwaka 2022 wanatajia kuongeza ufaulu Kwa Madarasa ya mitahani ambapo alisema kuwa wanatarajia kufaulisha wanafunzi Kwa daraja la kwanza na la pili tu na kuongeza ufaulu kutoka asilimia 93 Kwa kidato Cha pili , asilimia 94 Kwa kidato Cha Nne na asilimi 100  Kwa kidato Cha Sita ya Mwaka 2021.

Pamoja na hayo aliishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kwa kuwapatia miradi ya maendeleo kwa kujenga vyumba sita vya Madarasa kwani imesaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia hivyo kupelekea wanafunzi kusoma mahali pa zuri na kuongeza kiwango Cha taaluma shuleni hapo.

Shule ya Sekondari Iguguno ilianzishwa Mwaka 2000 ikiwa ni shule ya kidato Cha kwanza hadi cha Nne, na mnamo Mwaka 2016 shule hiyo iliongezewa hadhi ya kuwa na kidato Cha tano na sita kwa michepuo ya Sanaa Kwa tahasusi za HGK, HGL na HGE na Kwa Sasa ina jumla ya wanafunzi 1,124 kati ya hao wavulana ni 502 na wasichana wakiwa 623 ,kati ya hao ni wanafunzi 109 wanatarajia kufanya mtihani wa kidato Cha Sita Kwa Mwaka 2022 ikiwa wavulana ni 70 na wasichana 39.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.