• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Vifaa vyenye zaidi ya sh. Mill 143 kuchochea Uchumi Kwa jamii ya Wahadzabe.

Imewekwa kwenye: June 21st, 2022

Jamii ya wawindaji na wafugaji ya Wahadzabe  iliyopo katika kijiji cha Munguli Kata ya Mwangeza wilayani Mkalama imepokea vifaa kwaajili ya ufugaji  wa nyuki vyenye  thamani ya zaidi ya shilingi Milion miamoja Arobaini na Tatu(Tsh mill. 143.3)ili kuwasaidia katika ufugaji wa kisasa na kuacha ufugaji wa kienyeji kama walivyozoea.


Akikabidhi vifaa hivyo katika Kitongi  cha Kipamba  Kijiji cha Munguli  Mkuu wa wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo alisema kuwa vifaa hivyo vikawe chachu ya kuboresha ufugaji wao na kujiongezea kipato pia kuongeza uzalishaji wa zao hilo kwani ni chakula na ni dawa pia.


‘’kwa namna  ya kipekee niwashukuru wadhamini kutoka Mfuko wa  Kimataifa wa mazingira kwa Kinyiramba wanaitwa (Global Environmental Facility) kudhamini mradi huu  na kutoa zaidi ya Millioni mia kwenye mradi na kuhakikisha tunapata maendeleo endelevu huku  tukitunza mazingira ,ni jambo kubwa,  pia niwashukru Ofisi ya Makamu  wa  Rais  wizara ya Muungano na Mazingira kuona ipo haja na sisi wanamkalama kupata mradi mkubwa kama huu pamoja na kuwa tuna sifa za kuwa na msitu lakini Tanzania ina Misitu mingi jamani ni jambo la kipekee sana’’ Aliongeza Dc Kizigo.


Aidha Dc Kizigo alitumia fursa hiyo kuitaka jamii hiyo kutunza vifaa walivyopokea leo ili viwanufaishe kwani serikali imewekeza fedha nyingi  kuhakikisha wanapata faida na kuongeza uzalishaji ili inapofika mwisho wa mradi huu wawe wameweza kujitegemea na kukuza mtaji kwa  masilahi mapana ya jamii hiyona wilaya kwa ujumla .


Afisa Mazingira wilaya ya Mkalama Amon sanga amesema kuwa  jumla ya Mizinga 1100 imekabidhiwa  pamoja na vifaa vya urinaji asali vitakavyosaidia  jamii ya Wahadzabe kufuga nyuki na kurina asali  kisasa ili kuongeza  thamani  ya uzalishaji wa zao  la Asali ambalo linategemewa na jamii hiyo kama chakula pamoja na dawa .


‘’Wilaya ya Mkalama ni miongoni mwa wilaya Tano zinazotekeleza mradi wa kurejesha Ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula  katika maeneo kame Tanzania ambazo ni Nzega ( Tabora)  Magu ( Mwanza) Kondoa (Dodoma) pamoja  Micheweni (Kaskazini Pemba –Zanzibar) na katika wilaya zote hizo tano wilaya ya Mkalama ndio imepata bahati na hii inatokana na ukweli tu kwamba wilaya ya Mkalama imekidhi  vigezo vya kuwa na Msitu  wakutosha  na wenyenye ushawishi  mkubwa,  wilaya ya Mkalama ina msitu wa Hekari elfu moja mia sita hamsini na sita katika kitongoji cha Kipamba kijiji cha Munguli.’’ Alisema Sanga.


Aliongeza kuwa huo ulikuwa ni ushawishi tosha kwa wafadhili wa mradi kuona kuwa walengwa watanufaika ma mradi huo moja kwamoja ukizingatia katika kijiji cha Munguli kuna jamii ya Kabila la Wahadzabe ambao wanategemea zao la asali kama chakula.


Kabla ya  zoezi la kukabidhi vifaa hivyo Afisa nyuki wilaya ya Mkalama  Abdul  Alli alieza matumizi ya  vifaa hivyo kuanza hatua ya kuingia nyuki  hadi kuvuna zao la asali pamoja na namna ya kuchakata ili kupata asali yenye ubora  bila kuathiri kizazi ya chuki kilichopo  huku akitaja faida za kufuga nyuki kitaalamu itaongeza uzalishaji wa zao hilo kuvuna zaidi ya mara tatu kwa mwaka ambayo itaongeza thamani ya zao hilo na kukuza kipato kwa  Vikundi vya uzalisha , familia  pamoja na jamii kwa ujumla.


Mwenyekiti wa jamii ya Wahadzabe  Edward  Mashimba  ameishukuru serikali kupitia mradi wa kurejesha  Ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula kwa kuwajali na kuona jamii hiyo inafaa  kuwa na mradi endelevu na kusema  ni upendeleo wa kipekee kwa  serikali kuwekeza zaidi ya Million mia moja  kuhakikisha wanaingia katika dira ya dunia ambapo ameahidi kulinda vifaa hivyo ili viwasaidie katika kuongeza tija kwenye zao la asali na kuacha kufuga nyuki na kuvuna kienyeji jambo lililopelekea  kuua zao la nyuki  kwasababu walikuwa wanachoma moto nyuki  ndipo wapate asali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.