Mwenyekiti wa TCCIA Wilaya ya Mkalama, Bw. Milangton Musa Gunda, leo Desemba 22, 2025, ameongoza kikao cha Kamati ya Wilaya ya Mkalama, Kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliupo Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya.
Katika kikao hicho wajumbe wamejadili fursa mbalimbali za kiuchumi zitakazonufaisha wananchi wa Mkalama na maeneo ya jirani.
Miongoni mwa Fursa hizo ni pamoja na mradi wa uchakataji wa madini ya shaba ( copper) unaofanywa na muwekezaji , Tembo Mining and Resources, katika kijiji cha Ilongo.
Aidha kikao kimejadili mradi wa uzalishaji kokoto unaotarajiwa kutekelezwa katika kijiji cha Ishenga, ambako kuna miamba mingi ya granite inayofaa kwa uzalishaji huo. Mradi huo ukikamilika unatarajiwa kuzalisha tani 20 za kokoto kwa saa 1.
Vilevile wajumbe walijadili fursa ya kilimo cha mkonge, ambalo ni zao lenye faida mara mbili kwani linaweza kulimwa kwa mfumo wa mseto bila kuathiri uzalishaji wake.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa TCCIA Mkalama Akizungumza wakati wa kikao, Bw. Gunda alisema kuwa mambo yote yaliyojadiliwa ni ya manufaa makubwa kwa Wilaya ya Mkalama, akisisitiza kuwa wilaya ina fursa nyingi za kiuchumi, ikiwemo uwepo wa madini kama shaba (copper). Aliwashauri wananchi kuchangamkia fursa hizo kwa kuwekeza vizuri ili kuleta maendeleo endelevu.
Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuweka utaratibu rasmi wa kuwatambua na kuwasajili wachimbaji wadogo wadogo wa madini, ili shughuli zao ziwe halali, salama na zenye tija kwa wananchi na wilaya kwa ujumla.
OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582
Anuani ya Posta: P.o. Box 1007
Simu ya Mezani: 026-2964005
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz
Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.