• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SINGIDA AIPONGEZA WILAYA YA MKALAMA KUJIBU HOJA ZA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Imewekwa kwenye: June 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge ameipongeza menejimenti ya halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa namna walivyojibu hoja za mkaguzi  Mkuu na mdhibiti wa hesabu za serikali jambo alilotaja kuwa ni ushirikiano Mkubwa kwaajili ya masilahi ya wilaya na Mkoa kwa ujumla.

 Rc. Mahenge alisema hayo mapema leo katika kikao cha Baraza la madiwani la hoja lilifanyika katika ukumbi wa sheketela uliopo  halmashauri ya wilaya ya Mkalama.

‘’Halmashauri ya wilaya ya Mkalama sina maneno mengi   kwa sababu mnafanya kazi nzuri na moja ya kipimo cha kazi nzuri iko kwenye ukusanyaji wa  mapato, na  mwezi wa tatu kulifanyika tathimini ya mapato  kati  ya halmashauri zilizofanya vizuri Mkalama nayo ilikuwepo  hii inadhihirisha  kuwa mnafanya kazi kwa kushirikiana na hadi sasa mna asilimia 95% ya ukusanyaji wa mapato  niwapongeze sana kwa  kazi nzuri mnayoifanya’’ Aliongeza Rc Mahenge.

Hata hivyo aliagiza watumishi wote wa halmashauri kuwa na taarifa ya fedha zote zilizotumika kwenye miradi na kuzisambaza kwa madiwani ili wajue fedha zilizotumika katika kata zao  na kurahisisha ufuatiliaji kwa kila hatua.

Pamoja na hayo aliendelea kupinga vikali suala la Wanganga wa jadi wanaotumia ramli chonganishi  ( LAMBALAMBA)  wilayani  hapa  kuwa vitendo hivyo ni  kinyume na  sheria za Nchi kwani wanapita kwa wananchi na kuwachangisha fedha  ili kuwatibu suala hilo halikubaliwi kwani linavunja amani  na kuchochea chuki kwa wananchi.

Hata hivyo aliwaagiza madiwani kusimamia suala hilo kwenye Kata zao huku akitoa onyo kali kwa yeyote atakayekiuka agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo alitumia fursa hiyo kuwataka madiwani pamoja na viongozi mbalimbali wilayani Mkalama kuwasisitiza wananchi kutunza  akiba ya  chakula walichonacho  ili wilaya isije ikakubwa na njaa kutoka na mvua kunyesha chini ya wastani hivyo kupelekea  baadhi ya maeneo kuwa na uhaba wa chakula.

Awali akisoma taarifa Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Asia Messos alisema kati yahoja 51 zilizoibuliwa na Mkaguzi mkuu wa serikali  tayari  27 zimejibiwa kikamilifu huku zingine 24 zikiwa hazijabiwa kikamilifu na kuongeza  kuwa Menejimenti ya wilaya ya Mkalama imejipanga kikamilifu kujibu hoja hizo huku wakihakikisha wanaziba mianya ya kuibuliwa kwa hoja mpya.

Diwani wa kata ya Mwangeza Bosco Samwel ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama alisema kuwa uongozi wa wilaya ya Mkalama kwa kushirikiana na wataalamu mbalimbali wilayani hapa watahakikisha wanafanya kazi kwa kushirikiana ili kuongeza ukusanyaji wa mapato  na kuendelea kupata hati safi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.