• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

ONGEZENI UZALISHAJI WILAYANI MKALAMA 'RC SERUKAMBA'

Imewekwa kwenye: November 9th, 2023

ONGEZENI UZALISHAJI WILAYANI MKALAMA ' RC SERUKAMBA '


Mkuu wa  Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba amewataka Wananchi wa Kijiji Cha Hilamoto , Dominiki , Munguli , Mwangeza na Ikolo  Kata ya Mwangeza Wilaya ya Mkalama kuongeza maeneo ya Kilimo katika kipindi cha Kilimo Ili kuongezea uzalishaji Wilayani hapa na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Wilaya na Mkoa kwa ujumla.


Amesema hayo mapema Leo Novemba 09, 2023 katika ziara yake ya kukagua Miradi ya Maendeleo ,  kusikiliza na kutatua kero za Wananchi aliyoifanya leo Wilayani hapa.


Aidha Mhe. Serukamba amesema lengo la serikali ni kuhakikisha Wananchi wanakuwa na uchumi mzuri pamoja na huduma muhimu Kwa kusogeza  huduma karibu ikiwepo pembejeo za Kilimo ambapo aliwasisitiza Wananchi kuendelea kujisajili katika daftari Ili waweze kununua mbolea ya ruzuku kwa bei ya punguzo.


Amesema kuwa lengo la kuongezea uzalishaji kwa wakulima ni kupambana na hali ya umasikini Mkoani hapa na kuwaeleza endapo Kila Mkulima ataongeza maeneo ya kulima watapelekea kukua kwa Uchumi pamoja na kuboresha maisha yao.


"Niwasihi Wananchi ongezeni maeneo ya kulima, tulime alizeti kwa wingi, Kitunguu , Mahindi, dengu na mazao mengine Ili Mkoa wetu uwe katika hali zuri ya uchumi " Alisisitiza Serukamba .


Pia amewataka kulima Kilimo cha kisasa na chenye tija kwakutumia mbolea pamoja na mbegu bora ili kuongezea uzalishaji.


Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kutatua kero mbalimbali za Wananchi ndio maana anapita kijiji kwa kijiji kuhakikisha kero za Wananchi zinatatuliwa  kama sio  kumalizwa kabisa.


"Serikali inatatua kero za wananchi ndio maana Leo mnaniona nipo hapa " Alisisitiza Serukamba Rc Singida.


Pamoja na hayo ametumia mikutano hiyo kuwataka Wananchi kuacha kuuza mazao  yakiwa Shambani na kuwataka kujiunga kwenye vyama vya ushirika Ili kuwa na bei elekezi itakayowafanya madalali kukosa soko kwani wamekuwa wakiwatumia wakulima hao kujinufaisha wenyewe.


Sanajari na hayo amewataka Wananchi Wilayani Mkalama kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa mlipuko wa homa ya kutapika na kuharisha ( Kipindupindu) kwa kuzingatia usafi wao binafsi na mazingira yao wanakoishi kwakuwa na vyoo bora.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.