Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhe. Moses Machali, ametoa wito kwa watumishi wa serikali na wadau mbalimbali kuongeza ushirikiano katika kutekeleza shughuli za maendeleo wilayani Mkalama. Ametoa wito huo wakati wa Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Mkalama (DCC) kilichofanyika Desemba 10, 2025 katika ukumbi wa Sheketela uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama. Katika hotuba yake, Mkuu wa Wilaya amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama pamoja na menejimenti yake kwa kusimamia kwa ufanisi miradi ya maendeleo na kuhakikisha mapato ya Halmashauri yanasimamiwa ipasavyo.

Aidha, wadau waliohudhuria kikao hicho—wakiwemo viongozi wa dini, wawakilishi wa vyama vya siasa na wadau wa sekta binafsi—wameupongeza uongozi wa Wilaya ya Mkalama kwa kuendelea kudumisha amani na kusimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na zisizo za serikali, viongozi wa vyama vya siasa, sekta binafsi pamoja na viongozi wa dini.
OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582
Anuani ya Posta: P.o. Box 1007
Simu ya Mezani: 026-2964005
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz
Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.