• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru wazindua miradi ya Maendeleo wilayani Mkalama

Imewekwa kwenye: August 10th, 2022
  1. Mwenge wa Uhuru 2022 umezindua rasmi  miradi  mbalimbali ya Maendeleo wilayani  Mkalama.


Miradi ya Maendeleo iliyozinduliwa ni pamoja na mradi wa madarasa Saba katika shule ya Sekondari Gumanga yaliyotekelezwa kwa  fedha za Uviko 19 uzinduzi wa daraja la mawe katika kijiji Cha Minganga Kata ya Miganga , mradi wa Maji Milade Kata ya Tumuli, Uwekaji jiwe la Msingi katika kituo Cha Afya Gumanga ambayo imegharimu jumla ya TSH.Bilioni 1.34.


Pamoja  na kuweka Mawe ya Msingi na kukagua miradi, Mwenge umetembelea na Kuzindua kilabu ya kupinga rushwa katika shule ya Sekondari Nduguti pamoja na kutembelea program ya lishe shule ya Sekondari Gumanga, Mapambano dhidi  ya Maralia na VVU na UKIMWI na kukagua  kikundi cha Vijana cha Iguguno .


Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Bw. Sahili Nyanzabara Geraruma ameupongeza uongozi wa wilaya  ya Mkalama Katika kutekeleza miradi ya Maendeleo vizuri huku akiwataka kufanyia kazi mapungufu yaliyobainika kwenye baadhi ya miradi.


 Akiongea katika uzinduzi wa daraja la Mawe kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Geraruma amewataka wahandisi kuendeleza teknolojia  ya mawe na wengine waige kwani amesema kuwa linatumia   kiasi kidogo Cha fedha ikilinganishwa  na mengine yanayojengwa kwa zege na nondo.


Aidha amewataka wananchi kuitunza miundo mbinu ya miradi yote iliyozinduliwa  Leo  Kwa Maendeleo yao pamoja na kulitunza daraja  kuondoa uchafu na kulinda vyuma visiibiwe Ili kuondoa  changamoto ya upitikaji wakati wa mvua Kama ilivyokuwa mwanzoni.


Hata hivyo amewataka wahandisi wa tarura ambao ndio wasimamizi wa Ujenzi wa daraja hilo kuweka viakisi mwanga ili kuzuia ajali ambazo zinaweza Kutokea wakati wa usiku.


 Mkuu wa Wilaya ya Mkalama  Mhe. Sophia Kizigo alieleza umuhimu wa miradi yote  kuwa itatatua changamoto mbalimbali za wananchi  ikiwepo kutatua kero  ya Upatikanaji Maji safi salama katika kijiji cha Milade pamoja na  changamoto waliyokua wakipata wananchi wa kata ya Miganga waliokuwa  hawezi kwenda Hospitali ya Wilaya kwa Sababu ya kukatika Kwa mawasiliano  ya barabara na kusema  kukamilika Kwa daraja hilo litawasaidia watu wa   Nkinto, Miganga  na Nduguti Katika Shughuli zao za kibiashara na kijamii.


Kwa upande wake Mhandisi wa TARURA wilaya ya Mkalama  Mang'ara Magoti Matiku amesema Ujenzi wa daraja hilo imegharimu Tsh. Milioni 180.5 na kuokoa TSH.milioni 639.4 kwa kuwa Kama lingejengwa  kwa zege na nondo lingegharimu TSH.milioni 820.


 Mhandisi Magoti amesema fedha hizo zimetolewa na Serikali kupitia fedha za mfuko wa jimbo kwa mwaka 2021/22 na unatekelezwa na Mkandarasi Chase Investment  wa mwanza na kazi zilizopangwa ni kuchimba kupanga mawe kushuka Chini kumwaga zege na kujenga mawe.


Pamoja na hayo Kiongozi wa mbio za mwenge  Sahili Nyanzabara Geraruma  aliwasisitiza Wananchi kushiriki katika sensa  ya watu na  Makazi kujitokeza kuhesabiwa  tarehe 23 .8.2022, pia kukomesha na kutokomeza Maralia Kwa kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga, kupiga vita dhidi ya madawa ya kulevya , Mapambano  ya rushwa pamoja  na  wanachi kuzingatia masuala  ya Lishe Ili wawe na afya  njema.


 Mwenge wa Uhuru umepokelewa Wilayani Mkalama Leo ambapo umekimbizwa kilometa 129 na umekagua miradi mitano na programu tano.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA TATHMINI YA LISHE ROBO YA NNE – WILAYA YA MKALAMA 2025

    September 03, 2025
  • KONGAMANO LA HUDUMA ZA KIFEDHA WILAYANI MKALAMA

    August 19, 2025
  • MWENGE WA UHURU, WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 36 MKALAMA 2025

    July 21, 2025
  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.