• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mradi wa Shule Bora waanza kuimarisha mifumo kwakutoa mafunzo kwa Viongozi wa Elimu .

Imewekwa kwenye: September 27th, 2022


 MAAFISA ELIMU TAALUMA, TSC, WADHIBITI UBORA ELIMU  NA WARATIBU ELIMU KATA , WANOLEWA NA SHULE BORA.

 Katika kuboresha elimu wilayani Mkalama Mradi wa shule bora umetoa mafunzo  endelevu kwa walimu kazini (MEWAKA)  kwa  Maafisa Elimu taaluma, Wadhibiti Ubora elimu, TSC , pamoja na  Waratibu elimu kata ili kubadili mitazamo ya walimu  na kupelekea matokeo chanya.

Mafunzo  hayo  yamefanyika   kwa siku moja  katika Shule ya Msingi Nduguti  iliyopo Kata ya Nduguti Wilayani Mkalama.

Mwezeshaji wa  Mfunzo hayo  Jasie Sijjo alisema kuwa lengo la mafunzo  ni kuwajengea uwezo  Viongozi hao na kuwa  chachu kwa  walimu jambo  ambalo litawasaidia  kujua namna ya ufundishaji  na  kuwasaidia walimu kuwa na elimu shirikishi kwa  na jumuishi kwa kuzingatia  wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

‘’Miongoni mwa Malengo ya program ya Shule bora ni kuimarisha mifumo na leo tumeanza na nyie viongozi  tukiamini mtapeleka chachu kwa walimu  ambayo itapelekea  kubadili mitazamo yao na kuleta matokeo chanya’’ Alisema   Sijjo.

Aidha  Bw. Sijjo aliongeza kuwa  mradi wa Shule bora unatekelezwa kwa Mikoa tisa Nchini ambayo imegundulika kuwa na changamoto katika sekta ya Elimu  na unatarajia kuwafikia  wanafunzi takrabani  Milioni Nne.

‘’mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka Saba na utawafikia wanafunzi  takribani  Millioni  Nne , Walimu Elfu  Hamsini  na  Nne , Shule Elfu tano  Mia saba hamsini na Saba pia  mabadiliko na ubunifu  yataonekana na kutathiminiwa katika ngazi za chini  ambazo walengwa muhimu watapatikana katika Shule zote za Msingi Nchini’’. Aliongeza Bw. Sijjo.

Naye Bi. Telise Msongole  mwezeshaji  katika Program ya Shule Bora  aliwaelekeza  Viongozi  namna ya kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kama njia ya kujisomea  na kupata habari mtandaoni na nakuongeza kuwa  MEWAKA inaenda kufanikiwa kutokana na Viongozi hao kuwa waadilifu  katika  kipindi chote cha mafunzo .

‘’ kiongozi ni kuonyesha njia naamini  usikivu huu na uamanifu mliounyesha Mewaka inaenda kuleta matokeo chanya kwa walimu wetu kwani viongozi mmepokea na mtaaenda kuwarithisha walimu na kupelekea matokeo chanya kwa wilaya yetu ya Mkalama na Mkoa kwa ujumla.Aliongeza Bi.Msongole.

Akiongea kwa niaba ya washiriki wote Mratibu  elimu  Kata ya Kinampundu  Abubakari  Misanga  aliishukuru serikali kupitia program ya Shule bora kwa mafunzo hayo kwani yamewajengea uwezo  nao watakuwa chachu kwa walimu wote ili kuhakisha kiwango cha elimu kinakuwa katika Mkoa wa Singida hivyo kuleta matokeo Chanya ka maslahi mapana ya wilaya na Mkoa  wa Singida.

Program ya Shule Bora inatekelezwa kwa  Mikoa ya Kigoma, Katavi, Simiyu, Singida, Rukwa, Mara, Dodoma,Tanga pamoja na Pwani  na unafadhiliwa na serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UK aid  na gharama za mradi zitakuwa  na bajeti ya Paundi za Kiingereza 89 Millioni, sawa na Shillingi Billioni 270 za Kitanzania  na utafanya  katika  ngazi zote za mradi ,Mradi huu unatekelezwa hadi ifikapo  mwaka 2027.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.