• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkalama bila UKIMWI inawezekana

Imewekwa kwenye: December 2nd, 2021

Katika kupambana na ugonjwa wa UKIMWI ni muhimu kila mtu kuzingatia  kwa dhati elimu na ushauri wanaopata kutoka kwa wataalamu ,Viongozi wa serikali na viongozi  wa dini wa kujiepusha na mambo mbalimbali yanayowaingiza katika ushawishi na kuwapelekea kufanya maamuzi yasiyosahihi yanayowapelekea kwenye hatari ya kupata Maabukizi ya UKIMWI.

Hayo yamesema katika maadhimisho ya siku ya  UKIMWI Duniani ambayo hufanyika Disemba Mosi ya kila mwaka na ambapo kiwilaya ilifanyika katika Kijiji cha Ishinsi Kata ya Msingi.

Akimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Mkalama, Afisa Tarafa wa Tarafa ya Nduguti  Bw. Remigius Ngole  amesema kuwa katika kupambana na janga la Ukimwi jamii inatakiwa kujiepusha na vitendo  vinavyochochea kujamiana ikiwa ni pamoja na ulevi uliopitiliza  pamoja na utumiaji  wa madawa ya kulevya .

‘’UKIMWI upo Duniani kote na maambukizi yapo Zaidi kusini mwa Jangwa la Sahara  na Tanzania ni moja ya nchi  zilizopo eneo hilo .Mkalama sio Kisiwa hivyo mfahamu kwamba UKIMWI upo wilaya ya Mkalama , na hali ya maambukizi ya UKIMWI  Kiwilaya kwa kipindi cha January hadi Oktoba ni 2.1% hivyo nawasihi tuendelee kuchukua hatua Madhubuti ya kupambana na ugonjwa wa UKIMWI’’.aliongeza Bw.Ngole.

Awali akisoma risala kwa Mgeni Rasmi Mratibu wa Ukimwi  Halmashauri ya wilaya ya Mkalama Bw. Zakaria Lupindo amesema kuwa  kuna umuhimu mkubwa wa jamii kuendelea kuelimishwa ili kufahamu umuhimu wa kupima  afya zao  ili wanaogundulika kuwa na maambukizi  ya VVU kuanza kutumia dawa za kufubaza makali ya VVU.

Katika hatua nyingine Bw.Lupindo ameishukuru serikali kuongeza vituo vya Tiba na Mafunzo (CTC) kutoka vituo 5 vivyokuwepo mwanzo hadi 10 kwani imesaidia kusogeza huduma  ya tiba na  matunzo kwa wanaoishi na VVU  ndani ya wilaya ya Mkalama  ambapo kwa vituo vyote 10 upatikanaji wa dawa ni 100%  ambayo imepunguza usumbufu wa kufuata dawa Nje ya wilaya.

Pia amesema kuwa timu ya uendeshaji afya wilaya hasa waratibu wa UKIMWI  wamefanya juhudi za kuhamasisha na kutoa elimu na kuweza  kupima  wananchi afya zao ambapo kwa kipindi cha January hadi Oktoba jumla ya watu 16,092 ambapo wanaume walikuwa ni 6,324 na wanawake ni 9,770 walipima  afya zao na kutambua afya ,walikutwa na  na maambukizi ya VVU ni 343 wanaume 136 na wanawake 207 sawa na asilimia 2.1 ya Maambukizi  huku walionza huduma ya tiba na mafunzo wakiwa ni 342.

Kila ifikapo tar 1/12ya kila mwaka Tanzania huungana na mataifa yote Duniani kufanya maadhimisho ya siku ya UKIMWI ikiwa na lengo la kutoa elimu ya kujikinga na VVU pamoja na kutathimini hali ya maambukizi ya virusi  vya UKIMWI  na kupata mapendekezo ya njia bora za kufanya ili kudhibiti maambukizi mapya VVU.

Kauli mbiu ya mwaka  huu ni ‘’ZINGATIA USAWA ,TOKOMEZA UKIMWI ,TOKOMEZA MAGONJWA YA MLIPUKO.’’ikiwa na lengo la kuhimiza usawa  katika jitihada zote zinazochukuliwa katika  mapambano dhidi ya UKIMWI  na magonjwa mengine ya  mlipuko ikiwemo ugonjwa wa homa kali ya mapafu yaani UVIKO 19.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.