• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mbunge viti maalumu agawa kg 550 za Mbegu ya Alizeti ili kuunga Mkono juhudi za Serikali .

Imewekwa kwenye: November 18th, 2021

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Singida Mhe.Aysharose Mattembe amegawa  kilogramu Mia tano hamsini  za mbegu ya  Alizeti (Kg550) aina ya Record (Standard) kwa  Wanawake wa wilaya ya Mkalama  ili kuunga mkono juhudi za Serikali ya kuongeza tija katika uzalishaji wa zao la Alizeti Mkoani Singida.


Zoezi hilo lilifanyika  hivi karibuni katika ukumbi wa Ofisi za Chama cha mapinduzi (CCM) Kijiji cha Nduguti kata ya Nduguti wilayani Mkalama katika ziara yake ya Kikazi ya kutembelea  Wanawake  wa  Mkoa wa Singida .


Aidha Mhe.Matembe alisema kuwa serikali imekua ikitumia Fedha nyingi kuagiza mafuta ya kula nje ya Nchi  ndio maana ikaja na mkakati wa kuongeza tija katika uzalishaji wa zao hilo kwa Mikoa ya Dodoma, Simiyu  na Singida ya kuhakikisha zao la alizeti linalimwa kwa wingi ili mafuta yapatikane kwa wingi Nchini.


Pia amewataka wanawake kufanya kazi kwa bidii na kuongeza uzalishaji kwa maslahi mapana ya familia, wilaya na Taifa kwa ujumla.


“Naipongeza serikali yetu kuona ipo tija ya kuongeza uzalishaji wa  zao la Alizeti nimeona nami niiunge mkono serikali yangu sikivu  kwa kugawa mbegu hizi kwa wanawake hawa ninajua wanawake ndio wazalishaji wakuu hivyo ninawaombea mbegu hizi zikamee na kazaa vizuri ili kuongeza pato lenu wanawake na familia zenu kwaujumla’’. Aliongeza Mhe.Mattembe.


Awali akitoa elimu ya kilimo cha zao la hilo , Afisa kilimo wilaya ya Mkalama Bw.Daniel Jacobo  alisisitiza kanuni bora za kilimo cha alizeti , ambazo ni  kupanda kwa wakati, kutumia   mbolea za Asili na za Viwandani kupalilia kwa wakati huku wakiwataka  kuwatumia wataalamu pindi wanapoona mimea yao haipo kwenye hali ya kawaida.


Akitoa neno la shukurani kwaniaba ya wanawake hao Diwani wa viti maalumu  wilaya ya Mkalama Mhe.Mariam Kahola alimshukuru Mhe.Mbunge kwa kuwatembelea wanawake wa wilaya ya Mkalama na kuwapatia mbegu  za alizeti ili kuongeza uzalishaji wilayani Mkalama ambapo aliongeza kuwa watatumia elimu ya kilimo   vizuri kwa kulima zao la  alizeti  na kuzingatia  kanuni bora za kilimo  katika kukuza pato la wilaya na taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.