• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Makamu wa Rais azindua Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya Mkalama

Imewekwa kwenye: February 19th, 2019

Muda mfupi uliopita Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewahutubia wananchi wa Wilaya ya Mkalama katika Mkutano uliofanyika kwenye moja ya viunga vya Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Mhe. Samia ambaye aliambatana katika ziara yake aliambatana na mawaziri watatu,  alianza ziara hiyo kwa kukagua miundombinu ya shule ya sekondari Iguguno kabla ya kwenda kuangalia hatua ya ujenzi wa daraja la mto Sibiti na alihitimisha ziara hiyo muda mfupi uliopita kwa kuzindua Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama na kuzungumza na wananchi.

Akizungumza kabla ya hotuba ya Mhe. Makamu wa Rais, Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe. Elias Kwandikwa alisema kuwa dhamira ya serikali kwa sasa ni kuhakikisha wananchi wa Wilaya ya Mkalama hawapati changamoto yoyote kutokana na ubovu wa miundombinu ya barabara na ndio maana kwa kushirikiana na Wakala wa barabara wa Taifa (TANROADS) itahakikisha kila upande unaunganishwa kwa kiwango cha lami.

“Hivi karibuni tutaenda kujenga daraja la chuma pale kijiji cha Msingi na wakati wowote fedha ikipatikana kipaumbele chetu kitakuwa ni kuweka lami barabara inayotoka Iguguno hadi daraja la Sibiti huku tukiunganisha pia barabara ya lami kutoka kijiji cha Gumanga hadi Msingi” Alisisitiza Mhe. Kwandikwa.

Kwa upande wake Naibu waziri wa Maji Mhe. Juma Aweso alisema kuwa mpaka sasa zaidi ya shilingi bilioni 10 zimeshatumika kwa miradi ya maji ya Wilaya ya Mkalama ikiwa ni pamoja na mradi wa maji wa Kikhonda, Ipuli, Iguguno, Nyahaa na Nduguti ambapo alisisitiza kuwa fedha za miradi hiyo yote zilishalipwa na wananchi wameanza kupata huduma ya maji kwa miradi iliyokamilika.

“Lakini Mhe. Makamu wa Rais ni lazima niseme ukweli kuwa mradi wa maji wa Nyahaa umejaa ufisadi mkubwa sana kwa sababu serikali imelipa zaidi ya shilingi milioni 900 lakini mradi huo haujakamilika mpaka sasa ingawa mkandarasi alishalipwa hela zote na cha kusikitisha zaidi mhandisi aliyekuwa anasimamia mradi huo amehamishiwa Gairo” Alitoa angalizo Mhe. Aweso

Kufuatia hali hiyo Mhe. Aweso alimuomba Makamu wa Rais kumuagiza katibu Mkuu wa Wizara ya Maji amuandikie barua ya wito mhandisi huyo ili afike kwenye kikao cha majumuisho ya Ziara keshokutwa na kutoa majibu ya kina kuhusu suala hilo ombi ambalo Mhe. Makamu wa Rais alilikubali.

Katika hotuba yake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliwapongeza viongozi wote wa Wilaya ya Mkalama kwa kukamilisha ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ambapo aliwataka kuendelea kufanya hivyo katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya na miradi mingine ya serikali.

“Lakini lazima niseme ukweli kuwa kitendo cha kusimamishwa pale Ibaga kimeonesha wazi kuwa kuna ukosefu wa ushirikiano baina ya wananchi kwa sababu inaonekana kuna baadhi ya watu wanapangwa kusimama barabarani na mabango kwenye misafara ya viongozi jambo ambalo si zuri na linachafua taswira nzuri mliyoijenga wananchi wa Mkalama” Alisisitiza Mhe. Samia.

Mhe. Samia alihitimisha hotuba yake kwa kuwasihi wananchi wa Mkalama kutunza mazingira hasa katika kipindi hiki cha Masika ili vyanzo vya maji vilivyopo visikauke na kusababisha ukame wakati wa Kiangazi.

“Mwisho ninawaomba Wananchi wa Mkalama na Mkoa wa Singida kwa ujumla, tujihadhari sana na ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu japo sijapata takwimu ya Wilaya lakini takwimu ya Mkoa si nzuri hata kidogo hivyo tujilinde dhidi ya Ugonjwa huu hatari ndugu zangu” Alimalizia Mhe. Samia.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.