• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

JESHI LA UOKOAJI NA ZIMA MOTO LAWAPIGA MSASA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA

Imewekwa kwenye: June 1st, 2023


Jeshi la zima moto na uokoaji Mkoa wa Singida wametoa mafunzo kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Makalama ya namna ya kudhibiti na kujiokoa yanapotokea majanga ya moto wakiwa ofisini hata majumbani.


Mafunzo haya yamefanyika mapema leo Juni 1 2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambapo yalijumuisha Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na watumishi wote wa  Makao Makuu ya Halmashauri ya  Wilaya.


Akiongea wakati akifungua mafunzo haya Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bw. Abdalla Njelu amesema mafunzo haya yatawajengea uwezo watumishi namna ya kutumia vidhibiti moto pindi majanga ya moto yapotokea wakiwa ofisini hata majumbani kwani wengi wao walikuwa hawajui namna ya kutumia vifaa hivyo.

‘’Tumepata taarifa jana kuwa mnakuja kwaajili ya kutoa elimu kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama , kweli leo hii mmekuja kwaajili ya mafunzo naimani elimu hii itawasaidia sana maana najua wengine wanaiona tu ‘fire extinguisher’ lakini hawajui hata kuitumia’’ Aliongeza Bw. Njelu.


Pamoja na hayo  Bw. Njelu amewataka kutumia elimu waliyoipata leo kuwa mabalozi kwa wengine pamoja na kutoa msaada wa dharura pale yanapotokea majanga ya moto.


Sajini wa Kituo SSGT. Boniface Wamlamba amesema kuwa jeshi la zima moto na uokoaji linafanya kazi kwa mujibu wa sheria namba 14 ya mwaka 2007 kabla ya kufanyiwa marekebisho ya mwaka 2021 ambayo inafanya shughuli ya kuokoa maisha, kuzima moto pamoja na kusoma ramani za nyumba na kutoa ushauri kabla ya kuanza ujenzi na kutoa huduma kwa jamii.


SSGT. Wamlamba amesema mafunzo wanayotoa yatamsaidia mtu kujua kinga ya tahadhari ya majanga ya moto na vithibiti moto vipi vinapaswa kutumiwa kutokana na aina ya moto kabla ya kutoa taarifa kwenye jeshi la uokoaji na zimamoto kupitia namba yao ya dharura 114.


Akiongea kwaniaba ya watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ,Afisa Maendeleo ya Jamii Bw. Atiki Mohamed amelishukuri Jeshi la Uokoaji na zima moto Mkoa wa Singida kwa mafunzo waliyoyatoa leo ambayo yamewapa dira, elimu na namna ya kufanya inapotokea dharura ya moto ambapo ameahidi watatumia elimu hiyo adhimu kuelimisha jamii  namna ya kutumia vithibiti moto hivyo kulingana na madaraja ya moto.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.