• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii imetakiwa kuwekeza kwenye Elimu

Imewekwa kwenye: July 28th, 2022

Jamii  imetakiwa  kuwekeza kwenye  elimu  ili kujenga kizazi cha  wasomi  na kinachoweza kujitegemea , pia kuleta  mageuzi   ya kiuchumi , Kifikra ,kwenye jamii na taifa kwaujumla.


Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia  Kizigo amesema hayo July 28 2022  katika mahafali ya darasa la saba katika shule ya  Awali  na Msingi  Nduguti  (NPPEMS) yaliyofanyika mapema leo shuleni hapo katika  Kijiji cha Nduguti kata ya Nduguti  Wilayani Mkalama.


Aidha Mhe. Kizigo alisema kuwa elimu ni msingi wa kila kitu endapo jamii itawekeza katika elimu  itatengeneza  jamii  yenye uwezo mkubwa wa kupambanua mambo mbalimbali  na kujenga kizazi cha wasomi kitakacho kuwa msaada mkubwa kwa taifa.


Pamoja na hayo aliupongeza uongozi wa Shule ya awali na Msingi Nduguti kufanya vizuri katika mitihani ya darasa la nne na kusema matokeo hayo yanatoa dira chanya kwa matokea ya darasa la saba hivyo kuwata watahiniwa hao kujiandaa kikamilifu na masomo ya  Sekondari kuweza  kuingia kwenye ulimwengu wa wasomi wenye ushindani mkubwa.


Dc Kizigo aliwapongeza  wazazi kwakushirikiana   na walimu katika kuboresha taaluma shuleni hapo huku akiwataka wazazi kufuatilia maendeleo ya watoto wao ili  kutambua watu wanao  Mshirikiana na watoto , kuwa fahamu vizuri tabia zao na mienendo yao.


Awali akisoma Risala kwa mgeni Rasmi mkuu wa  Shule hiyo   Mwl Jackline Mushy  alisema  maendeleo ya taaluma shuleni hapo yamekua  yakiridhisha kwani toka mwaka 2019  hadi 2021 matokeo ya darasa la Nne wamekua wakifaulisha kwa asilimia mia moja (100)

Aidha  Mwl Jackline alitaja ufaulu huo mzuri unachangiwa na juhudi za wazazi , walimu  , Wanafunzi pamoja na  Maafisa  elimu  ambao wamekuwa wakifuatilia  kwa ukaribu  maendeleo  ya shule hiyo ambapo aliahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa maslahi mapana ya wilaya ya Mkalama na Taifa kwa ujumla.


Pamoja na mafaniko hayo Mwl Jackline alitaja changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo ikiwa ni pamoja na  ubovu wa miundo mbinu ya barabara ya kwenda shuleni  , kutopewa nafasi katika ziara za kimasomo, pamoja na ushirikishwaji duni wa vikao vya taaluma vinavyofanyika wilayani hapo .


Sanjari na hayo aliwashukuru wazazi na walimu kwa ushirikiano wanaouonesha na kuunga mkono juhudi zinazotolewa na shule hiyo ambapo amesema wataendelea kutoa elimu bora  kuhakikisha taaluma wilayani hapa inakua  na kuunga mkono juhudi za serikali za  kuboresha sekta ya Elimu Nchini.


Shule ya awali na  Msingi Nduguti ina takribani ya wanafunzi mia mbili (200) kati ya hao wanafunzi 18 ni  watahiniwa wa darasa la Saba na wanatarajia kufanya mitihani yao ya kuhitimu  mapema mwezi wa kumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.