• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Hali ya Upatikanaji wa Maji safi na salama wilayani Mkalama Sasa ni asilimia 67.17

Imewekwa kwenye: June 16th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo amezitaka jumuiya za watumia Maji wilayani hapa kuwapa muda wahasibu wanaoajiriwa kwenye jumuiya zao ili kujiridhisha na Utendaji kazi wao huku akiwaonya kuacha kupeana kazi kwa kujuana.


Aliyasema hayo June 15 mwaka huu wakati akihutubia Katika mkutano Mkuu wa Mwaka wa wadau wa Maji wilayani Mkalama.


Aliendelea kusema kuwa ili jumuiya zifanye vizuri lazima ziwe na malengo na usimamizi mzuri wa miradi ya maji huku elimu ikiendelea kutolewa kwa jamii ya namna ya kutunza miundo mbinu ya maji ili iweze kumnufaisha Kila Mwananchi na kutatua kabisa tatizo la upatikanaji Maji wilayani hapa.


"Ninakupongeza Meneja pamoja na jumuiya za watumia maji hakika mnafanyaje kazi nzuri sana hadi Sasa  hali ya upatikanaji Maji safi na salama wilayani ni asilimia 67.17 na hapa tupo 2022 naimani ikifika Mwaka 2023 uhakika wakufikisha asilimia 85 utakuwepo na tukiendelea hivi kabla ya mwaka 2025 tutakua tumefikia asilimia 100". Aliongeza Dc Kizigo.


Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maji Wilaya Mkalama Meneja wa RUWASA Mhandisi  Antidus Muchunguzi  alianza kwakuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutenga Bill 2.3 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwaajili utekelezaji a miradi ya maji wilayani Mkalama kuwa bajeti hii itachochea kuongeza upatikanaji wa huduma ya Maji na kutimiza adhima ya  Serikali ya kumtua Mama ndoo kichwani.


Aliendelea kusema hadi Sasa RUWASA Wilaya ya Mkalama imehuisha na kusajili vyombo vya watumiaji Maji 20 huku akisema wanaendelea na kazi ya kuunda na kusajili jumuiya kwa miradi ya Nkungi pamoja Kinampundu inayotarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni Mwaka huu.


Muchunguzi alisema kwa Mwaka 2021/2022 ofisi ya RUWASA Wilaya ya Mkalama ilipanga kuchimba visima 11 katika vijiji vya Nkalakala, Nkungi, Matongo, Nkinto, Mwangeza Lukomo, Mwanga, Ilunda, Kinankamba na Kisuluiga na tayari visima vinne  vimechibwa katika vijiji vya Malaja, Nkalakala , Iambi na  Mdilika huku  Mkandarasi akiwa yupo site na kazi inaendelea.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama James Mkwega alizitaka jumuiya kutembea kwenye malengo na kuleta mabadiliko katika jamii huku akisema haina haja kuendelea kufanya kazi kwa jumuiya ambazo hazifuati sheria na taratibu za uendeshaji .


Upatikanaji wa Maji wilayani Mkalama Kwa Sasa ni asilimia 67.17 sawa na Wananchi 161,405 wanapata huduma ya Maji kati ya wananchi oye 240,299 na huduma hii hutokana na vyanzo vya Maji chini ya Ardhi ambavyo ni visima virefu, vifupi na vya kati.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.