• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

ZIARA YA KATIBU MKUU CCM KULETA NEEMA YA VITUO VYA AFYA WILAYANI MKALAMA

Imewekwa kwenye: March 2nd, 2023


Katibu Mkuu wa Chama  cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Daniel Chongolo ameahidi vituo viwili vya Afya Wilayani Mkalama pamoja na kujenga Wodi ya Mama na Mtoto katika kituo cha Afya Kinyangiri  ili kuhakikisha  wananchi wanapata matibabu bora katika maeneo yote Wilayani hapa.

Ametoa kauli hiyo Leo March 2 2023  katika ziara yake ya kikazi Wilayani Mkalama yenye lengo la kuimarisha Chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/2025 kuhakikisha pesa zilizotolewa na Serikali zinafanya maendeleo yaliyokusudiwa na yenye tija kwa Wananchi.

‘’ Nimetembelea kituo cha Afya cha  Kinyangiri pamoja na Hospitali ya Wilaya ambayo tayari mmeanza kupata huduma hapo nimeona Kituo cha Afya ni cha miaka ya themanini huko, sasa ninaenda kuongea na Mama nimwambie umenituma Mkalama nimegundua kuna upungufu wa Vituo vya Afya nyie niachieni kazi hiyo kituo kingine kitaenda Iguguno na kingine mtachagua wenyewe ni wapi kipelekwe’’ Aliongeza Chongolo.


Pamoja na hayo amewataka Watumishi wa Afya kuendelea kutoa huduma nzuri kwa Wananchi kutokana na uchache wao  huku akisema kuwa Serikali inatambua upungufu wa Watumishi  uliopo Nchini na  imekuwa ikiajiri kadri ya uwezo ili kuhakikisha wanatatua changamoto za Watumishi  ili kuboresha  huduma.


Akiongea na wananchi wa Kata ya Iguguno na Nduguti Ndg. Chongolo aliwataka Wazazi kuwekeza kwenye elimu kwa kuhakikisha Watoto wanapata elimu iliyo bora kwani Serikali inatoa elimu bila malipo kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha Sita  ambayo imekusudia  Taifa kuwa na kizazi cha wasomi watakao shika nafasi mbalimbali hapa Nchini.


Pamoja na hayo Ndg. Chongolo amesema kuwa ataongea na wanaohusika na masuala ya Miundombinu ya Barabara kuhakikisha Wananchi wa Wilaya ya Mkalama wanajengewa Barabara ya kiwango cha Lami kutoka Iguguno kupitia Makao Makuu ya Wilaya Nduguti ambayo itafika hadi Sibiti  inayounganisha Mikoa ya Simiyu, Manyara na Arusha.


Awali akitoa taarifa katika Mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali alieleza kuwa Wilaya iko salama na Wananchi wanaendelea na shughuli mbalimba za uzalishaji mali na uchumi .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WILAYANI MKALAMA

    June 16, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkalama Apongeza Ujenzi wa Zahanati ya Nkenke

    June 13, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA SINGIDA

    June 11, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.