• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wilaya ya Mkalama kupunguza mlipuko wa Ugonjwa wa kichaa cha Mbwa kutoka 8% mwaka 2019 hadi 4%mwaka 2020/2021

Imewekwa kwenye: September 26th, 2021

Katika kuelekea kilele cha wiki ya  kichaa cha Mbwa duniani, Zaidi ya Mbwa Mia tatu na Hamsini (350) wamepatiwa chanjo ya kichaa cha Mbwa katika Vijiji vya  Maziliga na Nduguti Kata ya Nduguti wilaya ya Mkalama Mkoani Singida.

Zoezi hili limefanyika kuanzia tar 25 katika Kijiji cha maziliga na kumalizika  Mapema leo September 26, 2021  Kijiji cha Nduguti  katika Ofisi ya Kijiji cha Nduguti  Ambapo Wafugaji wamesisitizwa Kupeleka Mbwa wao kupatiwa Chanjo ili kuwakinga na madhara yatokanayona ugonjwa huo  pindi Mbwa wao wanapopata ukichaa.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali Linalojihusisha na usitawi wa Wanyama (Education for African Animals Walfare) Bwana Ayubu Nnko Amesema kuwa Jamii ione Umuhimu wa Kuchanja Mbwa wao ili kuepusha hasara zitakazowapa   pindi Mbwa wao wanapopata ugonjwa na kung’ata Binadamu, Ambapo ametaja kwa nchi za Afrika na Tanzania ikiwemo kuwa kila mwaka hutumia Zaidi ya Dolla milioni ishirini kutibu watu waliopata ugonjwa wa kichaa cha Mbwa.

“Shirika la Education for Animals Walfare Tumekuwa tukishirikiana na Wilaya ya mkalama Tangu Mwaka 2019 ambapo kulikuwa kunaripotiwa matukio  ya mara kwa mara ya mlipuko wa ugonjwa wa kichaa cha Mbwa , na Tanzania huungana na Dunia nzima kuazimisha chanjo ya Kichaa cha Mbwa kwa mwezi Septemba na Kilele chake huwa ni Septemba 28 kwa kila mwaka hivyo niwasihi wafugaji kutumia fursa hii adhimu kuleta Mbwa wenu wapate chanjo na chanjo hii inatolewa bure. ” Ameongeza Ayubu Nnko Mkurugenzi(EAAW).

Afisa mifugo wilaya ya Mkalama Bw. Dotto Michael  ameishukuru Serikali kupitia Shirika la Education for Animals Walfare(EAAW) kuleta chanjo kwa wilaya ya mkalama tena bure kwaajiri ya kuchanja Mbwa hivyo kuwataka Wananchi kujitokeza kwa wingi kuleta Mbwa kupatiwa chanjo ili kuunga mkono juhudi za serikali.

Aidha Bw Michael ameongeza kuwa zoezi hilo limesaidia kupunguza Ugonjwa wa Mlipuko wa kichaa  cha Mbwa kutoka 8% kwa mwaka 2019 hadi kufikia 4% kwa mwaka 2020/2021  kwa wilaya ya Mkalama na ambapo amesema kuwa zoezi hilo ni endelevu na kwa mwaka 2021/2022 wanatarajia kufikia 2% ya kupunguza mlipuko wa Kichaa cha Mbwa.

 Daudi Samsoni na Saimon Willium ni miongoni mwa wafugaji wa Mbwa ambapo wameishukuru serikali kuona haja ya kuwapelekea chanjo kwenye maeneo yao na kutoa chanjo hiyo bure kuwa ni fursa ya kipekee ambapo wameahidi kuwalinda na kuwatunza Mbwa wao  vizuri kwakuwapa chakula na kuwajengea mabanda mazuri kwani Mbwa ni Rafiki wa Binadamu na Askari wazuri wa Nyumbani.

Kilele cha maadhimisho ya Kichaa cha Mbwa ni September 28.2021 huku kauli mbiu ikiwa ni “CHANJA  MBWA WAKO NA PAKA WAKO MARA MOJA KWA MWAKA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA,KUMBUKA UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA HAUNA TIBA”.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.