• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wiki ya maji yafikia tamati leo Mkalama

Imewekwa kwenye: March 21st, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka leo amewaongoza Wananchi wa Wilaya hiyo kwenye maadhimisho ya wiki ya maji yaliyofanyika katika kijiji cha Iguguno.

Maadhimisho hayo yaliambatana na uzinduzi wa visima viwili vya  Maji vyenye thamani zaidi ya shilingi milioni 15 vilivyojengwa kwenye kijiji cha Iguguno shamba na Sofia.

Wakati wa uzinduzi huo Mhe. Masaka aliwataka wananchi wa vijiji hivyo kuhakikisha wanatumia maji hayo kwa utaratibu mzuri ili waweze kujihakikishia kupata huduma hiyo kwa muda mrefu zaidi.

“Pia naomba mtunze mazingira katika maeneo yote yanayozunguka vyanzo hivi vya maji ikiwemo miti tuliyopanda leo kwa sababu mazingira haya yakiwa mazuri hata uhakika wa upatikanaji wa maji katika maeneo yenu utakuwa ni mkubwa” Aliongeza Mhe. Masaka.

Akisoma hotuba yake ya kuadhimisha kilele cha Wiki ya Maji mbele ya wananchi wa kata ya Iguguno Mhe. Masaka aliipongeza jumuiya ya watumiaji wa Maji pamoja na serikali ya kijiji cha Iguguno kwa kutambua umuhimu wa maji safi kwa jamii inayoizunguka na kuamua kuchimba visima kwenye kijiji cha Iguguno Shamba na Sofia kupitia fedha zao za makusanyo yanayotokana na watumia maji.

“Lakini pia katika miundombinu ya maji iliyopo, vituo vya kuchotea maji pamoja na pampu za mikono vilivyopo ni 736 ambapo vinavyofanya kazi ni 519 huku 217 vikiwa havifanyi kazi hivyo nakuagiza Mhandisi wa maji uhakikishe vituo hivyo vinafanya kazi kabla ya mwezi juni na ikilazimu hata wananchi wenyewe wachangie gharama za utengenezaji wa pampu hizo” Alisisitiza Mhe. Masaka.

Katika taarifa yake aliyoisoma mbele ya wananchi kwenye maadhimisho hayo, Kaimu Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Mkalama Mhandisi Antidius Muchunguzi alisema kuwa Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika halmashauri ya Wilaya hiyo kwa sasa imefikia asilimia 61 ikiwa ni sawa na wananchi 129,750 kati ya wananchi 213,674 iikiwa ni ongezeko la asilimia 20 zaidi ya miaka mitatu iliyopita huku akibainisha kuwa kuwa lengo kubwa la idara yake ni kuhakikisha wananchi wote wanaoishi Wilayani hapo wanapata huduma ya maji safi na salama.

Maadhimisho ya Wiki ya Maji kwa mwaka huu yaliambatana na zoezi la upandaji miti 400 kwa vyanzo vya maji vya Nduguti, Kinyangiri, Kikhonda na Iguguno na yalibeba kauli mbiu isemayo “Hakuna atakayeachwa: kuongeza kasi ya upatikanaji wa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa wote katika dunia inayobadilika kitabia nchi”.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.