• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WASAIDIENI WAFUGE KISASA ' RC SERUKAMBA '

Imewekwa kwenye: May 28th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida , Mhe. Peter Serukamba  ameagiza ofisi ya Mkurugenzi kupitia Idara ya Mifugo kuhakikisha wanawatembelea na kujua maendelea ya hali ya ufugaji kwa kikundi cha Tunza kilichopo Kijiji cha Nduguti Kata ya Nduguti Wilayani Mkalama ili waweze kufuga kisasa na kuweza kujikwamua kiuchumi.


Ametoa maagizo hayo Mei 27 wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya kikundi hicho ambacho kinajishughulisha na ufugaji, Kilimo, kununua mazao mbalimbali pamoja na kulea watoto yatima wapatao watano.


‘’Ninakuagiza Afisa Mifugo wilaya kuwatembelea wanakikundi ili muweze kuwashauri namna ya kufuga kisasa waweze kupata maarifa ya ufugaji bora na wenye tija pia kama walivyoomba wasaidieni kuwapatia elimu ya ujasiriamali’’ Aliongeza Rc Serukamba


Aidha amewapongeza wanakikundi kwa juhudi wanazozifanya kuhakikisha wanatumia fedha vizuri wanazopewa na Serikali kwakujiendeleza na kujikita katika uzalishaji mali pamoja na kurejesha kwa wakati fedha hizo ambapo pia amesema vikundi hivi vinapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu ili vifanye vizuri Zaidi kwa maslahi mapana ya wanamkalama.


Katika hatua nyingine Mhe. Serukamba amewataka wanakikundi kuhakikisha wanakata bima ya afya kwaajili ya familia zao ili inapotekea changamoto ya Mwanafamilia ameugua ziweze kuwasaidia kwani suala la afya ni muhimu kwa familia na jamii kwa ujumla.


Awali akisoma taarifa kwa Mkuu wa Mkoa Mwenyekiti wa Kikundi cha Tunza Bi. Asha Kiula amesema kikundi kinajishughulisha na shughuli za uzalishaji mali ikiwemo ufagaji , Kilimo pamoja na kununua na kuhifadhi mazao na kuuza pindi bei inapokuwa nzuri ili kujipatia faida na kuongeza mtaji wa kikundi.


Bi Kiula ametaja mafanikio waliyopata  kuwa ni pamoja na kupata faida ya kujiinua kiuchumi kwa mwanakikundi mmoja mmoja ambapo wameishukuru serikali kupitia Wizara ya maendeleo ya jamii , jinsia wanawake na makundi maalumu kuendelea kutoa mikopo ya asilimia Nne (4%) kwaajili ya wanawake, na fedha hizo wanakopeshwa na  Halmashauri kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii na  kwa  riba nafuu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WILAYANI MKALAMA

    June 16, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkalama Apongeza Ujenzi wa Zahanati ya Nkenke

    June 13, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA SINGIDA

    June 11, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.