• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WATAKIWA KUTUNZA MIRADI YA MAENDELEO KWA VIZAZI VYA BAADAE.

Imewekwa kwenye: November 10th, 2022

Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya Wilaya ya Mkalama Bi. Asia Messos amewapongeza wananchi wa kijiji cha Mntamba  kwa kuchangia fedha katika  miradi ya maendeleo  na kujitolea  nguvu kazi  pamoja na mali zao.

Ameyasema hayo  leo  Novemba 9/2022  wakati  akikagua na kutembelea miradi  ya maendeleo iliyoibuliwa na wananchi hao  kwenye ziara yake ya kikazi inayoendelea Wilayani  hapa  ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja  na usimamizi wa matumizi ya fedha za wananchi kwa Vijiji vya Nkinto , Makulo  na Mntamba.

Aidha aliwataka wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji  kubuni vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuendelea kuchochea miradi ya maendeleo  pamoja na kuhakikisha wanaweka fedha hizo benki kwa usalama zaidi.

Pia aliwataka wananchi kuendelea kulinda na kuitunza miradi yote inayotekelezwa Wilayani hapa ili idumu kwa  vizazi vijavyo.

Katika hatua nyingine alikemea vikali suala la Lambalamba linalotaka kushamiri Wilayani hapa na kusema kuwa yeyote atakayebainika kushirikiana na waganga hao wajadi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake kwani vitendo hivyo vinachochea migogoro na uvunjifu wa amani  katika jamii.

Naye  Diwani  wa kata ya Nkito Mhe. Reuben Mhai aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kutoa fedha nyingi katika Kata hiyo kwaajili ya ujenzi wa Miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo alisema kuwa watahakikisha wanaunga mkono juhudi za Serikali kwa kusimamia vyema miradi hiyo na kuchangia katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Katika ziara hiyo aliungana na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kukagua Maendeleo ya ujenzi wa  darasa moja shule ya Sekondari  Nkinto, mradi wa Shule madarasa mawili (SM2)  Sekondari  ya Nkinto ,Ujenzi wa zahanati katika kijiji cha Makulo  , Ujenzi wa  Zahanati  kijiji cha Mntamba ambayo imejengwa kwa nguvu za Wananchi pamoja na Nyumba mbili za walimu kijiji cha Mntamba zilizojengwa kwa nguvu za wananchi.

Aidha Bi. Asia (Mkurugenzi Mtendaji) alizidi kuupongeza uongozi wa Serikali ya Kijiji cha Mntamba kwa ubunifu wao wa kujenga nyumba ambazo kimsingi zimegharimu kiasi kidogo cha fedha ikilinganishwa na miradi mingine ya iana hiyo.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.