• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi wapatao 2728 Wilaya ya Mkalama wamepatiwa chanjo ya UVIKO 19

Imewekwa kwenye: October 8th, 2021

Elimu ya chanjo ya UVIKO 19 inayoendelea kutolewa wilayani Mkalama imezaa matunda  baada ya wananchi wapatao 2728 kupatiwa chanjo hiyo.

Mratibu wa chanjo wilaya ya Mkalama Bw. Duncan  Kifaluka amesema kuwa wananchi wamepokea elimu na  na kuunga mkono hatua iliyofikiwa na serikali ya kutoa mafunzo kwa  ngazi ya taifa  hadi kuwafikia wananchi walipo ya kuwa wamepokea zoezi hilo kwa mtazamo chanya na kuchukua hatua ya kupatiwa chanjo.

‘’sisi  kama Wilaya  tulipokea dozi 3550 na kufikia sasa zimetumika Dozi 2940  ambayo imefanya  jumla ya Wananchi 2728 kupatiwa chanjo na hadi kufikia  leo tumebakiwa na dozi 610 tu na zoezi bado linaendelea “Ameongeza Bw. Kifaluka mratibu chanjo.

Katika hatua nyingine ameeleza kuwa  jitihada hizo  zimesaidia jamii ya Wafugaji , wakulima na wawindaji ya Wahadzabe Kutoka Kijiji cha Munguli na Vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi kupata chanjo  ambapo amesema takribani Wananchi mia moja(100) mpaka jana tar 7 /10 /2021 walipatiwa chanjo huku akisema zoezi hilo bado linaendelea  .

Kwa upande wake mwakilishi kutoka Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali na Serikali zamitaa (TAMISEMI) Idara ya jamii  na Lishe  Dinah Atinda ameeleza namna serikali inavyofanya jitihada za kupambana na janga la Corona na kuona umuhimu na  kutoa elimu kwa jamii  ili kila mtu aone umuhimu wa kuchanja kuepusha madhara  makubwa  zaidi .

Richard Magodi kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia ,Wazee  na Watoto ambaye alikuwa miongoni mwa waliofika katika Kitongoji cha Kipamba Kijiji cha Munguli kata ya Mwangeza kutoa elimu  juu ya chanjo,ameeleza namna alivyofurahishwa na muamko na Mapokezi  ya jamii hiyo kupokea zoezi la chanjo vizuri na kujitokeza kwa Wingi kupatiwa Chanjo ambapo ameeleza hii itasaidia kupunguza Vifo kwa Nchi na maeneo yote Duniani .

Miongoni mwa wananchi wa jamii ya Wafugaji , Wakulima na Wawindaji  ya Wahadzabe Bw Edward Mashimba na  Doricas James kutoka Kitongoji cha Kipamba  wamesema kuwa wamepokea chanjo kwa mikono  miwili na maelekezo yote yalitolewa na serikali na kujitokeza kupata chanjo ili wao wabaki salama huku wakiwashauri wengine wenye Imani potofu  kuhusu chanjo hiyo kwenda kuchanja ili kulinda maisha yao na jamii kwa ujumla.

Kampeni ya Chanjo ya UVIKO 19 Ilizinduliwa  Oktoba Mosi mwaka huu na Litaendelea hadi Oktoba 14 mwaka huu.




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WILAYANI MKALAMA

    June 16, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkalama Apongeza Ujenzi wa Zahanati ya Nkenke

    June 13, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA SINGIDA

    June 11, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.