• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

'WANANCHI TUUENZI MUUNGANO KWAKUFANYA KAZI KWA BIDII' AMESEMA DC MACHALI

Imewekwa kwenye: April 20th, 2023

MKUU wa Wilaya ya Mkalama , Mhe.Moses Machali, amewataka wananchi kuwa wazalendo na kuuenzi Muungano kwa kufanya kazi kwa bidii.


Aidha, amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwakulinda na kutunza miundombinu ya barabara isiharibiwe.

Ameyasema hayo leo April 20, 2023 wakati akizungumza na wananchi wa Kata za  Kikhonda na Nduguti kijiji cha Mwando kwenye mkutano wa hadhara  ikiwa ni maandalizi ya kuelekea maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.


Machali amesema wananchi wanatakiwa  kuonyesha uzalendo na kutii  sheria zinazowekwa na mamlaka husika ili kulinda na kutunza miradi  mbalimbali ikiwamo ya barabara kwani serikali inatumika fedha nyingi kuigharamia.


"Ninatoa maelekezo kwa yeyote atakayekutwa anaharibu miundombinu ya barabara kwa kupitisha ng’ombe au mkokoteni barabarani faini yake ni shilingi  elfu tano  kwa kila ng’ombe au kifungo cha mwaka mmoja jela au vyote kwa pamoja," alisema Mhe. Machali.


Amesema katika  kipindi cha  miaka 59 ya muungano, Tanzania inajivunia mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kutatua kero za muungano  kwa kuimarisha umoja, mshikamano  na usalama uliopo nchini.


Nao baadhi ya wazee waliokuwepo kabla na baada ya uhuru wamesema kuwa wanajivunia muungano kutokana na hapo awali huduma za jamii  hazikuwepo Wilayani Mkalama walilazimika kuzifuata  Wilaya ya Singida lakini sasa huduma zinawafuata hadi kwenye maeneo yao.


Walisema baadhi ya huduma wanazozipata sasa katika Wilaya ya Mkalama ni pamoja na uwepo wa Shule nyingi za Sekondari na msingi, barabara, umeme na huduma za afya ambazo sasa zinapatikana katika zahanati,vituo vya afya na hospitali ambazo zimejengwa na serikali.


"Maendeleo makubwa yamepatikana ndani ya muungano huu, hivyo tunaahidi kuwaenzi waasisi wa muungano  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume," wamesema wazee hao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.