• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

WAKURUGENZI WAPEWA NONDO KUONGEZA UKUSANYAJI WA MAPATO NDANI YA HALMASHAURI

Imewekwa kwenye: January 19th, 2023



Wakurugenzi wa Halmashauri  za Mkoa  wa Singida  wameshauriwa kufanya makisio sahihi ya mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na kuimarisha  ushirikishwaji  wa Wakuu wa Idara  na Vitengo katika ukusanyaji  wa  Mapato  ya ndani hatua itakayopelekea  ongezeko la mapato na  kuondokana na utegemezi kutoka Serikali  Kuu.


Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Msaidizi  sehemu  ya Menejimenti na  ukaguzi  Mkoa  wa Singida Bw. Evodius Katare  Hivi karibuni  katika kikao cha kufunga tathimini ya  vyanzo vya mapato ya ndani  ya Halmashauri  za Mkoa  wa Singida jijini Dodoma.


Bw. Katare amesema baadhi ya halmashauri zinakusanya mapato madogo ukilinganisha na hali halisi ya  vyanzo vya mapato vilivyopo katika Halmashauri husika na kupelekea  upotevu wa mapato ambayo yangetumika kuleta maendeleo.


‘’Inasikitisha sana kuona Idara ndani ya Halmashauri  zinakusanya fedha ndogo ukilinganisha  na Mshahara ,posho, motisha  wanazopewa , unakuta Afisa aliyeaajiriwa  kwa kazi inayoleta mapato kwa mwaka mzima anakusanya  Mil. 2 hii siyo Afya kabisa kwa Halmashauri’’ Amesema Katare.


Aidha aliongeza kwakuzitaka Idara zinazohusika na  ukusanyaji  wa  Mapato  kuwa makini na kujitoa  kwaajili ya kazi hizi  na kuwataka kufanya kazi kwa Moyo kuhakikisha hakuna upotevu wa mapato  na kuacha uvivu  unaopelekea kutojali ukusanyaji wa fedha za Serikali.


Bw. Rwakatare amewashauri  Wakurugenzi  kujifunza  na kubadilishana uzoefu  kwa Halmashauri zilizofanya vizuri  katika ukusanyaji wa  Mapato ya ndani  ili kuibua vyanzo vipya vya mapato  pamoja na kuona namna bora ya kuongeza mapato katika Halmashauri husika.


Akizungumza wakati wa kufunga kikao hicho Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini  Ofisi ya Rais-TAMISEMI  ambaye ni Mwenyekiti wa Timu ya Mkoa wa Singida Bi. Nteghenjwa Hosseah amesema  kuwa ofisi ya TAMISEMI  katika zoezi hili imegundua  kuna baadhi ya ushuru wanakusanya Halmashauri moja huku zingine zikiwa hazikusanyi, ambapo alisema   ufika wakati Mkoa uweke utaratibu wa Halmashauri zote kukusanya kwenye vyanzo vinavyofanana bila kuwa na utofauti.


Zoezi hili limetoa fursa kwa Wataalamu  wa Halmshauri za Mkoa wa Singida kupitia bajeti zao kwa kina , kuongeza wigo wa mapato , kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato na kuandaa bajeti yenye uhalisia.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.