• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wakulima kujiandaa mapema na msimu wa Kilimo ili kuongeza uzalishaji

Imewekwa kwenye: October 26th, 2022

Mkuu wa  Wilaya ya Mkalama Sophia Mfaume Kizigo amewataka wakulima kujiandaa mapema na msimu wa kilimo kwa kufuata njia  bora za kilimo ili kuwa na chakula cha kutosha na kukuza uchumi wao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo jana katika ziara yake ya kikazi ya kusikiliza na kutatua kero za  wananchi katika kijiji cha Ishinsi Kata ya Msingi Wilaya ya  Mkalama.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Wilaya Kizigo aliwataka wananchi kutumia fursa iliyotolewa na Serikali ya kusajili wakulima wote kwenye mfumo ili waweze kupata ruzuku ya mbolea  kwa bei nafuu.

‘’ninawashauri wakulima kujisajili ili mpate ruzuku ya mbolea, Serikali imesikia kilio chenu kutokana na bei ya mbolea kuwa juu sana , kuna faida kubwa sana za kukopeshwa mbegu na Serikali’’.

Hata hivyo aliwataka wananchi  kuibua miradi ili Serikali inapotoa fedha iwe rahisi kupeleka sehemu ambayo tayari  kuna kitu kinaendelea .

‘’Ninaomba wananchi muwe tayari kuanzisha maboma ili inapotokea tumepata fungu Serikalini iwe rahisi kupeleka sehemu yenye  mradi tayari, anayepewa lifti ni yule aliyepo barabarani’’ Aliongeza Dc Kizigo.

Hata hivyo, alisema kuwa serikali ya awamu ya Sita imelenga kutatua kero za Wananchi katika masuala ya Afya , Elimu ,Kilimo , Maji  , Umeme  na huduma hizo kumfikia Mwananchi popote alipo  kwa ustawi wa jamii.

Afisa kilimo , Mifugo na uvuvi  Wilaya ya Mkalama  Selemani  Msunga  alisema kuwa Serikali imekusudia kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya kilimo na sasa imeanza kuandikisha wakulima katika mfumo ili wapate ruzuku ya mbolea  na kusema hadi sasa Takribani Wakulima 7200 wameonekana kwenye mfumo na zoezi linaendelea huku akiwataka wakulima kuendelea kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hiyo.

Aidha, Bw. Msunga aliongeza kuwa Alizeti itabaki kuwa  zao la kimkakati wilaya ya Mkalama licha ya changamoto zilizojitokeza  Msimu wa Kilimo wa mwaka jana ambapo Serikali ilitoa mbegu ambazo hazikuwa na mavuno mazuri kwa wakulima na kuongeza kuwa kwa msimu wa mwaka huu 2022 Serikali itaendelea kutoa mbegu zilizo bora ili kuhakikisha zao la Alizeti linalimwa kwa wingi.

Baadhi ya wananchi wa kata ya Msingi walimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kufika kwenye maeneo yao ili kusikiliza kero zao na kutatua changamoto walizonazo wamesema wanaimani na serikali ya awamu ya Sita kuwa watawapelekea huduma nyingi za maendeleo ikiwepo  umeme kufika kila kitongoji ili wananchi waweze kukua kiuchumi na kukuza pato lao binafsi na Halmashauri.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.