• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wafugaji wametakiwa kuchanja Mifugo yao Ili kuwakinga na ugonjwa wa Mlipuko wa Kimeta

Imewekwa kwenye: July 6th, 2022

Wafugaji wilayani Mkalama wametakiwa  kujitokeza kwa  wingi kuchanja mifugo yao, kwani ufugaji wenye tija  ni ule unaolenga kuongeza ubora wa mazao yatokanayo na mifugo na kumnufaisha  mfugaji katika kukuza pato la familia, jamii na taifa kwa ujumla.


Mkuu wa wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo  amesema hayo mapema leo wakati akizindua zoezi la chanjo ya Mifugo dhidi ya ugonjwa wa Kimeta ,Chambavu  kwa Ng’ombe na  na Minyoo  na homa ya mapafu kwa mbuzi  na Kondoo katika kijiji cha Kinampundu , Kata ya Kinampundu wilayani Mkalama.


‘’Niwasihi  wafugaji kuhakikisha mnaleta mifugo yenu yote ili ipatiwe chanjo ili kuikinga na ugonjwa wa kimeta, na mtaalamu katuambia hapa kuwa ugonjwa huu  ni tishio kwa mifugo yetu  na kwa bindamu tusipuuze zoezi hili kwani wataalamu wamekuja kwenye maeneo yetu imebaki nyie tu kuleta mifugo hapa ili ichanjwe kuepuka madhara hayo’’. Aliongeza Dc Kizigo.


Pamoja na hayo ameagiza ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kuona namna ya kutafuta mbegu za majani ya malisho na kugawa kwa wafugaji , ili wapande kwenye maeneo ya malisho kwani kwakufanya hivyo itapelekea mifugo kupata majani ya kutosha na kuwa na afya bora hivyo kuongeza upatikanaji wa soko la mifugo na kukuza pato la wilaya.


Awali akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi Afisa Mifugo wilaya ya Mkalama Elias Mbwambo alisema kuwa zoezi hilo ni kutekeleza sera ya chama cha mapinduzi  na takwa la kisheria ambapo sheria ya udhibiti wa magonjwa namba 17 ya mwaka 2003 inaagiza mifugo yote ipatiwe chanjo ili kuzuia vifo vya mifugo  na ueneaji wa magonjwa ya Mlipuko kwa wanyama na binadamu, na usimamizi wa sera ya mwaka 2006 inayosisitiza ufugaji wa kibiashara wenye tija na ushindani wa kimataifa katika uvuvi na ufugaji ili kuunga mkono wafugaji wadogo waweze kuwa wajasiliamali wazuri.


Aidha Mbwambo aliongeza kuwa zoez hili ni endelevu katika wilaya ya Mkalama toka mwaka 2003  ambapo limekua likifanyika kila mwaka na limeleta mafanikio makubwa kwani vifo vitokanavyo na  magonjwa ya mifugo  vimepungua kutoka asilimia 22 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 4 mwaka 2021 huku  akitaja changamoto  kwa baadhi ya wafugaji kupuuza juhudi za serikali za kupambana na magonjwa ya mlipuko kwa mifugo yao na  kuficha mifugo  isipate chanjo  hivyo kupelekea hasara ndani ya familia na kwa wilaya pia.


Pamoja na hayo alisema kuwa  wilaya  imejipanga kuchanja  Ng’ombe 90,727  Mbuzi 79,158 , Kondoo 40,271 na zoezi hili litachukua takribani siku kumi na Nne  na watapita kwenye  Vitongoji vyote na Vijiji vyote vya Wilaya ya Mkalama.


Diwani wa Kata ya Kinampundu Silvester Marimo  alitumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa mpango wake kabambe wa kupambana na magonjwa yanayoikabili mifugo ambapo pia alisema watatumia fursa hiyo kuwahamasisha wafugaji kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo huku akiiomba Serikali  kuwajengea vibanio vya kudumu kwaajili ya kuingiza Ng’ombe wanapochanjwa kwani wanavyotumia sasa ni va kienyeji na sio vya kudumu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.