• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wafugaji wajikite kwenye soko la kimataifa-Masaka

Imewekwa kwenye: May 25th, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Mhandisi Jackson Masaka amewataka wafugaji waliopo Wilayani hapa kuhakikisha wanalisha mifugo yao katika maeneo waliyotengewa badala ya kuipeleka katika kila eneo la wazi wanaloliona.

Mhe: Masaka ameyasema hayo wakati akizindua zoezi la upigaji chapa Mifugo Wilayani Mkalama ambapo aliwashauri wafugaji hao kujiunga na vyama vya ushirika ili kufanya shughuli zao kwa faida tofauti na sasa ambapo kila mfugaji anafanya shughuli zake mwenyewe hali inayosababisha kutotengeneza faida kubwa.

“ Lakini pia baada ya kujiunga kwenye vyama hivyo tumieni sehemu ya faida mnayopata kuchangia shughuli za maendeleo kwa sababu maendeleo ya Wilaya hii yanaletwa na sisi sote kwa pamoja” Ameongeza Masaka.

Katika hatua nyingine Mhe: Masaka amewataka wafugaji hao kuhakikisha wanafuata taratibu za ufugaji wa kisasa ili mifugo yao iwe na afya kwa ajili ya kuanza kusafirisha nje ya Nchi.

“ Inawezekana nyama inayosifiwa na kuliwa nje ya nchi ikawa inatokana na Ng’ombe waliopo Tanzania hivyo ni vyema kuweka mifumo ambayo itatusaidia kupata faida pindi tukiuza mifugo yetu nje ya nchi” Amesema Masaka.

Amesema kuwa hatua ya kuuza mifugo hiyo kimataifa huwa inaanza pale Ng’ombe wanapouzwa katika soko la Mkoa wa Singida na hatimaye kusafirishwa mpaka nje ya Mkoa huo ambapo huko hukusanywa kabla ya kusafirishwa mpaka nje ya nchi.

Akizungumza mapema kabla ya kumkaribisha Mhe: Mkuu wa Wilaya, Afisa Mifugo na Uvuvi wa Wilaya ya Mkalama bw. Elias Mbwambo amesema kuwa pamoja na kuanza na tarafa ya Kinyangiri kwa mujibu wa ratiba, Zoezi hilo linatarajiwa kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.

“Katika zoezi hili mfugaji atalazimika kulipia shilingi mia tano kwa kila ng’ombe atakayepigwa chapa ili gharama hizo zitumike kufanikisha zoezi hili katika maeneo mengine tunayoendelea nayo na ng’ombe watakaohusika na zoezi hili ni kuanzia ndama wa miezi sita na kuendelea” Amesema Mbwambo.

Mbwambo amesema kuwa zoezi hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa sana udhibiti wizi wa mifugo kwani sasa mifugo itakuwa na alama inayoonesha ilipotoka na pia itasaidia katika harakati za udhibiti wa magonjwa ya mifugo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.