• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

UZINDUZI WA MBEGU ZA RUZUKU MKOANI SINGIDA

Imewekwa kwenye: October 6th, 2022

*Hakuna gharama usajili wa wakulima mfumo wa mbolea za ruzuku*


#wakulima watakiwa kujisajili kabla ya msimu wa kilimo kuanza


Imeelezwa kuwa usajili wa wakulima kwa ajili ya kunufaika na mbolea za ruzuku hauna gharama yeyote na yeyoye atakayewatoza kiasi chochote cha pesa wakulima atachumuliwa hatua.


Hayo yamesemwa Oktoba 5 2022 na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe wakati wa hafla ya kuzindua msimu wa kilimo kwa mwaka 2022/2023 uliofanyika katika ukumbi wa kanisa katoliki mkoani Singida.


Waziri Bashe ametoa pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Dkt. Stephan Ngailo kwa kusimamia na kuhakikisha Mfumo wa kielekitroniki wa mbolea za ruzuku unapatikana.


"Amesema awali jambo la kuwa na mfumo wa kuuza mbolea ya ruzuku lilionekana kuwa ni gumu lakini Dkt. Ngailo amelisimamia nankulifanya kuwa halisi" waziri Bashe aliongeza.


Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa  TFRA, Dkt.  Ngailo ametoa rai kwa wakulima wote nchini kujisajili kwenye ofisi za vijiji na vitongoji wanakofanyia shughuli za kilimo ili waweze kunufaika na mbolea za ruzuku zinazotolewa na Serikali kwa msimu wa kilimo 2022 /2023.


Amesema, serikali imetoa ruzuku za mbolea kwa msimu huu wa kilimo ili kunufaika na ruzuku ya mbolea ni lazima mkulima ajisajili na kueleza kuwa sharti kubwa la mkulima kusajiliwa ni kuwa na shamba, vinginevyo hakuna masharti mengine.


Aidha, Dkt. Ngailo amewataka wakulima kutoa taarifa sahihi juu ya ukubwa wa mashamba wanayoyalima ili kusaidia katika kununua mbolea itakayokidhi mahitaji kwani ukubwa wa shamba ndio utaamua ni kiasi gani cha mbolea unapaswa kununua.


Amesema, kwa sasa Serikali inawaandikisha wakulima kwa kuchukua taarifa zao za msingi ili waweze kupata huduma ya mbolea kwa wakati na kubainisha kuwa hapo baadaye wakulima watapigwa picha pamoja na kuchukuliwa alama za vidole ili kupunguza ubadhirifu unaofanywa na watu wasiokuwa waaminifu na hivyo kuwanufaisha wakulima hewa kwa mbolea za ruzuku.


Pia, Dkt. Ngailo alisema baada ya usajili huo wa awali, Serikali imedhamiria  kupita kwa kutumia GPS  katika maeneo waliyojiandikisha wakulima  ili kuhakiki ukubwa wa mashamba yaliyojazwa wakati wa usajili  na hivyo kuwataka wakulima kutoa taarifa sahihi za maeneo wanayolima.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.