• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Utaratibu ufuatwe wakati wa kuwasilisha migogoro-DC

Imewekwa kwenye: April 26th, 2018

“Kama umeshindwa kumsikiliza mama yako mzazi aliyekuzaa, utanisikiliza mimi Mkuu wa Wilaya?”

Hilo ni swali alilouliza Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka leo wakati wa maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambayo katika ngazi ya Wilaya yamefanyika katika kijiji cha Iguguno.

Mhe. Masaka ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo aliuliza swali hilo wakati akiwasisitiza wananchi wa Wilaya ya Mkalama kujenga utamaduni wa kumaliza matatizo yao wenyewe badala ya kusubiri viongozi wa serikali waingilie kwenye matatizo hayo.

“Ni aibu kwa watu wa familia moja kutegemea watendaji wa serikali kumaliza migogoro yao hivyo ni lazima kila mwananchi kwa nafasi yake ahakikishe anashiriki kikamilifu katika kutatua migogoro inayomkabili ndani ya familia yake” Alisisitiza Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka aliongeza kuwa kama matatizo hayo yataonekana kuzidi uwezo wa familia husika, ni vizuri hatua stahili za kushughulikia matatizo hayo zikafuatwa kwa kuanza kuyafikisha serikali ya kijiji, kata na tarafa kabla hayajafika katika ofisi yake.

Akitoa ujumbe wa maadhimisho ya Muungano ya Mwaka huu Mhe. Masaka amewataka wananchi kuhakikisha wanadumisha na kuuenzi Muungano huo huku akiwataka  kupuuza  kauli za baadhi ya watu wachache wanaobeza faida kubwa zinazopatikana ndani ya pande zote mbili za Muungano huo.

“Wewe Mwananchi wa Lukomo au Nyeri, una mashamba yako na umepata mazao ya kutosha, inakusaidia nini kuhoji kwanini Rais wa Zanzibar naye anapanda ndege?” Aliuliza Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka aliwasihi wananchi wote wa Wilaya ya Mkalama kuhakikisha wanalinda na kuitunza amani na utulivu uliopo hivi sasa huku akikisisitiza kuwa serikali haitafumbia macho aina yoyote ya viashiria vya uvunjifu wa amani vitakavyoonekana na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wahusika wote watakaoonesha viashiria hivyo.

Kuhusu kampeni ya kitaifa ya chanjo ya kujikinga na saratani ya Mlango wa kizazi inayoendelea hivi sasa kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 Mhe. Masaka amewataka wazazi wote kuhakikisha wanawapeleka watoto wao kupata chanjo katika vituo vitakavyotajwa ili kuwaepusha wasichana hao na tatizo hilo ambalo linazidi kuwa kubwa kila Mwaka.

“Kila Mwaka saratani ya mlango wa kizazi husababisha vifo vya wanawake zaidi ya 2000 nchi nzima hivyo asitokee mzazi yoyote kumkataza mwanae kupata chanjo hiyo kisa yeye hakuwahi kupatiwa kwa sababu miaka inabadilika na tatizo hili linazidi kuwa kubwa ndio maana Serikali imeamua kuchukua hatua” Alisisitiza Mhe. Masaka.

Mhe. Masaka alimalizia hotuba yake kwa kuwasihi wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi zinazooneshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dokta John Pombe Magufuli ambapo pia aliwataka waendelee kumuombea afya njema ili aendeleze jitihada za kuhakikisha Tanzania Mpya inasonga mbele.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.