• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

USHIRIKIANO UTALETA MATOKEO CHANYA KATIKA KUONGEZA UKUSANYAJI WA MAPATO

Imewekwa kwenye: July 10th, 2023

USHIRIKIANO UTALETA MATOKEO CHANYA KATIKA KUONGEZA UKUSANYAJI WA MAPATO MKALAMA' DC SAKULO MISENYI '


Kamati ya Fedha, Mipango  na Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wamekamilisha ziara ya siku mbili katika Mkoa wa Kagera yenye lengo la kutembele na kujifunza uwekezaji katika Sekta ya Viwanda, Kilimo pamoja na kujifunza namna ya kuongeza ukusanyaji wa mapato ambayo wamejifunza katika Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi Mkoani humo.


Ziara hiyo ilianzia katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Misenyi Mkoani Kagera ambapo Mkuu wa Wilaya hiyo Kanali, Wilson Sakulo amewataka kutumia ziara hiyo kuleta matokeo chanya katika Wilaya ya Mkalama , ambapo ametaja siri kubwa ya mafanikio ni ushirikiano baina ya Viongozi, Wataalamu pamoja na madiwani.


‘’ Ninapenda kuwahakikishieni wanamkalama kuwa hakuna muujiza mkubwa kama ushirikiano, mnatakiwa mkashirikiane baina ya viongozi wa Wilaya, Wataalamu pamoja na madiwani’’ aliongeza Kanali Sakulo


Aidha, Kanali Sakulo amewataka kusimamia vyanzo vya mapato walivyonavyo ili viweze kuleta mafanikio mazuri pamoja na kuongeza mapato ya Halmashauri ambapo pia aliwataka Waheshimiwa Madiwani kusimamia suala hili vizuri kwani wana muda mwingi wakukaa na wananchi kuwaambia umuhimu wa kulipa kodi kwa maslahi ya Wilaya.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi Mhe. Projestus Tegamaisho aliongeza kuwa Halmashauri ya Misenyi kwa  Mwaka wa fedha 2022/2023 ilijipanga kukusanya kiasi cha Shilingi Bilion 4.255 lakini hadi kufikia June 30 mwaka huu walifanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 6.085 sawa na 125% ambapo alisema kuvuka malengo hayo yanachagizwa na ushirikiano mkubwa kati ya Madiwani, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pamoja na  Ofisi ya Mkurugenzi.


Pamoja na hayo Mhe.Tegamaisho aliongeza kuwa mafanikio hayo pia yanatokana na mikakati mbalimbali waliojiwekea katika kufikia malengo ikiwa ni pamoja na uwepo wa Doria za kila siku (mchana na usiku), kuwepo kwa Vizuizi  katika maeneo maalumu ambayo wanakuwepo vibarua na mgambo pamoja na kutoa elimu kwa wafanyabiashara ambao ndio walipa kodi / Ushuru wa  Halmashauri.

@ded_mkalama @missenyidc @ortamisemi @

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.