• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Upatikanaji wa Maji safi na salama Kijiji Cha Milade kupunguza migogoro ya Familia

Imewekwa kwenye: July 29th, 2022

Imeelezwa kuwa upatikanaji wa Maji safi na salama katika kijiji cha Milade  Kata ya Tumuli utapunguza migogoro ya familia inayosababishwa na wakina Mama kutumia muda mwingi kutafuta Maji badala ya kuhudumia familia zao .

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo amesema hayo July 28 wakati akikabidhi mradi na kuweka jiwe la Msingi katika mradi wa Maji uliopo kijiji cha Milade  Kata ya Tumuli.

"Sasa mmepata mradi wa Maji ,mradi huu utapunguza zile kero, mama anaamka asubuhi anamuacha Baba kalala kitandani anafuata Maji umbali mrefu muda huo Baba anahitaji chakula unarudi umechoka mwisho wa siku Baba anaanzisha ugomvi kwa kuchelewa kurudi" aliongeza Dc Kizigo.

Aidha Dc Kizigo aliutaka uongozi wa jumuiya za watumia maji kuhakikisha wanasimamia vizuri mradi na kuweka pesa benki zitokanazo na mauzo ya maji kuepuka usumbufu wakukaa na pesa mkononi kwani inaweza kuwapelekea kutumia kwa matumizi yao binafsi.

Hata hivyo aliwataka Wananchi kupokea mradi huo na kuutunza,  kuchangia gharama za uendeshaji wa mradi  kwa kununua Maji Kwa ujazo wa  ndoo ya Lita 20 Kwa shillingi 40 na kuhakikisha wanatunza miundo mbinu ya maji kwa vizazi endelevu.

Katika hatua nyingine aliwataka Wananchi kushiriki katika zoezi la sensa ya watu na Makazi Agosti 23 Mwaka huu kwakutoa taarifa sahihi za familia zao ikiwepo taarifa za wenye ulemavu kwenye familia Ili kurahisisha utekelezaji kwa Serikali  kupanga mipango kulingana na mahitaji  sahihi kwa makundi Maalumu.

Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mkalama Mhandisi Antidus Muchunguzi alisema kuwa mradi huo umegharimu  Tsh. 502,000,000 na unatawanufaisha Wananchi wapatao 3060 wa kijiji cha Milade na kuongeza kuwa wamepokea maombi 100 ya kuunganisha Maji majumbani .

Mhandisi Muchunguzi Aliongeza kuwa kukamilika Kwa mradi huo utaongeza hari ya Upatikanaji Maji safi na salama Kwa asilimia 1.3 kiwilaya  na kupelekea Wananchi kukua kiuchumi kutokana na kuwa na muda mwingi wa uzalishaji Mali .

Mhe .Bilali  Msengi diwani wa Kata ya Tumuli aliishukuru Serikali kupitia Wakala wa Maji safi na usafi wa mazingira (RUWASA) kupeleka mradi wa Maji katika kijiji Cha Milade na kusema kuwa mradi  huo utawanufaisha wananchi kwa kupata Maji safi na salama pia kupunguza Magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya maji yasiyo safi na salama.

Pamoja na hayo ameahidi Kwa niaba ya wananchi kutunza miundo mbinu ya mradi huo na kuahidi  kupanua mradi ili adha ya upatikanaji Maji safi na salama kuwa historia katika kijiji cha Milade na Kata ya Tumuli Kwa ujumla.

Mradi huo umehusisha  ujenzi wa  Tenki la Lita 90,000 kwenye mnara wa mita 9 nyumba ya mashine Moja (1)  ulazazi wa  mabomba km 11.39 pamoja na ujenzi wa vituo 12 vya kuchotea maji.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.