• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

UONGOZI WILAYANI MKALAMA WATOA MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU (WAKOMA) 140

Imewekwa kwenye: December 23rd, 2022


Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya  Wilaya ya Mkalama  pamoja na Kanisa la Maranasa Kata ya Nduguti leo wametoa msaada wa chakula na mavazi  kwa wakoma  140 waishio katika Kijiji cha Nkungi ili waweze kusherehekea vema  sikukuu za Mwisho wa mwaka huu.


Akikabidhi vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Kizigo alisema kuwa msaada huo umelenga kuhakikisha wakoma hao wanasherehekea sikukuu kwa furaha ambapo amewatia moyo kwa kuwataka kutokata tamaa kutokana na changamoto waliyonayo na kuwatia moyo kwani matatizo waliyonayo kwani inaweza  kumpata yeyote.


‘’Leo tumekuja kuongea na nyie na kufurahi na nyie katika kipindi hiki cha kuelekea Mwisho wa mwaka najua mna changamoto nyingi lakini leo tumekuja kufurahi na sio kusikiliza changamoto’’. Amesema  Mhe. Kizigo


Mhe. Kizigo amebainisha kuwa wapo watu wenye ulemavu unaoonekana na usioonekana hivyo jamii inapaswa kuishi na watu hao kwa usawa na kutowanyanyapaa kwa namna yoyote.


"Nimedokezwa na Mwenyekiti wenu hapa kuwa mmetoka kujishugulisha hivyo niwapongeze sana kwani pamoja na hali mliyonayo bado mnajishughulisha na shughuli za uzalishaji mali ambazo kwa kiasi kikubwa zinachangia maendeleo ya Wilaya ya Mkalama na Taifa kwa ujumla" Ameongeza Mhe. Kizigo.


Kwa upande wao baadhi ya wanufaika wa msaada uliotolewa leo Bi Helena Samweli na Bw. Ilanda Salehe wameushukuru uongozi wa Wilaya ya Mkalama kwa kuwapelekea msaada huo na kuwasisitiza wasisite kufanya hivyo wanapopata nafasi  kwani kitendo hicho kimewafanya wajisikie wenye furaha na kuthaminiwa na Viongozi wa ngazi za juu.


Uongozi wa Wilaya ya Mkalama kwa kushirikiana na wadau wake mbalimbali umekuwa na utamaduni wa kuwatembelea na kupeleka misaada kwa jamii hiyo ambayo imekuwa ikiishi na changamoto ya kuathiriwa na Ugonjwa wa Ukoma kwa muda mrefu ambapo Msaada uliotolewa leo ni pamoja na Mahindi, Mchele, Sabuni, Sukari pamoja na nguo na Mashuka ya kujifunika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.