• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ujenzi wa hospital uanze wiki ijayo- Ndugulile

Imewekwa kwenye: October 31st, 2018

Viongozi mbalimbali wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameendelea na ziara za kikazi ndani ya wilaya ya Mkalama ambapo leo ilikuwa ni zamu ya Naibu waziri wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Daktari Faustine Ndugulile.

Mhe. Ndugulile aliipongeza wilaya ya Mkalama kwa jitihada za dhati za kuhakikisha wanapanda katika vigezo vya ubora wa utoaji wa huduma za afya au  “Star rating”  kama inavyojulikana kitaalam ambapo mwaka 2016  vituo vyote vilikuwa chini ya nyota 3 hali iliyoashiria hakuna kituo kilichokuwa kimekidhi viwango vya utoaji wa huduma bora.

“Lakini mwaka 2018 asilimia 33.5 ya vituo vilivyopo hapa Mkalama vimepata  nyota 3 au zaidi huku aslimia 66.5 ya vituo vikiwa na nyota 2 na hakuna hata kituo kimoja kisicho na nyota hivyo jambo lililoifanya Wilaya ya Mkalama kuwa ya tatu kwa mkoa wa Singida kwa upande wa utoaji wa huduma bora za Afya, hongereni sana” Alisisitiza Mhe. Ndugulile.

Akiwa katika eneo lililoandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya, Mhe. Ndugulile aliwapongeza wananchi wa kata ya Nduguti kwa kujitolea eneo kwa ajili ya kujenga hospitali ya Wilaya bila fidia yoyote ambapo aliwataka wananchi wa maeneo mengine nchini kuiga mfano huo.

“Kwa sababu tayari mmeshaletewa fedha za awamu ya kwanza na michoro mnayo ninaagiza ujenzi wa hospitali hii ya Wilaya uanze mapema wiki ijayo na kama kuna mtu atasema msubiri michoro mwambieni michoro hiyo aniletee mimi “ntadeal” naye lakini nyinyi anzeni kazi” aliongeza Mhe. Ndugulile.

Mhe. Ndugulile alimalizia ziara yake kwa kutembelea kituo cha afya cha Kinyambuli ambapo alizipongeza kamati zote zilizoshiriki katika ujenzi wa kituo hicho na kumuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kuhakikisha anatumia fedha za mapato ya ndani kumalizia kazi zote zilizobaki za ujenzi wa kituo kufikia mwisho wa mwaka huu ili kuanzia mapema mwakani wananchi waanze kupatiwa huduma katika majengo hayo mapya.

“Lakini pia niwatangazie wananchi wa Kinyambuli na Watanzania wote kuwa hivi sasa tumeanza kudhibiti dawa tunazosambaza kwa kuziwekea alama inayosomeka “MSD GOT” ambayo mbali na kuiweka nje ya maboksi ya dawa pia tumeiweka mpaka ndani kwenye tembe na kwenye bomba za sindano hivyo yoyote atakayeona vifaa tiba na dawa zenye alama hiyo zinauzwa kwenye maduka binafsi ya dawa tafadhali atoe taarifa kwenye mamlaka za Ulinzi na usalama” Aliongeza Mhe. Ndugulile.

Kwa mwaka 2018 serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetumia zaidi ya shilingi bilioni 5.3 kwa ajili ya ukarabati na uwekaji wa miundombinu ya Afya mkoani Singida ambapo pia imeuongezea Mkoa huo bajeti ya Afya kutoka shilingi bilioni 4 ya mwaka 2017/2018 hadi shilingi bilioni 7.5 kwa mwaka 2018/2019.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAKABIDHI KADI ZA MATIBABU BURE KWA WAZEE MKALAMA

    June 15, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA WILAYANI MKALAMA

    June 16, 2025
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkalama Apongeza Ujenzi wa Zahanati ya Nkenke

    June 13, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA SINGIDA

    June 11, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.