• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

TUMIENI MAFUNZO HAYA KUENDANA NA MABADILIKO YA MTAALA MPYA

Imewekwa kwenye: January 11th, 2024

Walimu wametakiwa  kusikiliza kwa makini na kujifunza namna mtaala mpya utakavyoenda kufanya kazi ili kuwasaidia kuendana na ,mabadiliko ya mtaala huo utakaoanza kutumika mwaka huu kwa madarasa ya awali hadi la tatu .

Akiongea wakati akifungua mafunzo kwa walimu katika Shule ya Msingi Nduguti iliyopo Kata ya Nduguti , Wilaya ya Mkalama  Mthibiti Mkuu ubora wa Shule Ignatus Kinyeje amesema kuwa mafunzo haya yakawe ni chachu ya kuleta mabadiliko katika taaluma huku akiwasihi walimu hao kuendana na mabadiliko hayo kwakuendelea kujifunza.


‘’Leo tunafungua mafunzo haya kwa naiaba ya mafunzo yote yanayoendelea leo Wilayani Mkalama ninawataka walimu kuwa na bidii katika mafunzo hayo pia mkipata fursa ya kusoma mkasomee masomo ya kifaransa na kichina kwani ndio yameongezwa katika mtaala huu mpya’’ Alisisitiza Kinyenje

Pamoja na hayo Mwl Kinyenje amewataka walimu hao kuwa na bidii katika ufundishaji katika kupandisha kiwango cha ufaulu wilayani hapa huku akiwataka kudhibiti suala la utoro kwa wanafunzi hususani katika kipindi hiki cha muhula mpya wa masomo kwa mwaka 2024.

Naye Kaimu Afisa Elimu Msingi Mwl. Amina Irumba aliwataka walimu hao  kuendana na mabadiliko ya Tekinolojia husani katika kipindi hiki cha kutumia (TEHAMA) shuleni na  kutumia mifumo mbalimbali katika kurahisisha utendaji kazi ambapo amesisitiza kuwa makini na taarifa zao za siri.

‘’ Ninawaomba walimu tuwe makini na taarifa zenu maana sasa mnatumia mifumo katika utendaji kazi wenu , wengi wetu bado hatuja ‘master’ kutumia mifumo hiyo mnapoenda huko ‘Stationary’ kuweni makini na taarifa zenu za siri hususani kutoa Nywira zenu’’ Alisisitiza Mwl Irumba.

Aidha Mwl Irumba  amewataka walimu kutumia vishkwambi walivyopewa kujisomea na kujifunza vitu mbalimbali kwaajili ya kuboresha utendaji kazi wao huku akiwaonya kuacha kutumia vishkwambi hivyo kwaajili ya kucheza michezo ya kubahatisha “ Kubet’

Sanjari na kuzindua mafunzo hayo timu hiyo ya Maafisa Elimu Wilaya pamoja na Uthibiti ubora Elimu Wilaya wamendelea kukagua hali ya uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza kwakutembelea Shule za Nduguti Shule ya Msingi, Gumanga, Ibaga, Mkalama pamoja na Shule ya Msingi Chemchem.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.