• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Fahamu jinsi TEA ilivyoboresha Elimu Mkalama

Imewekwa kwenye: September 20th, 2017

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ni chombo kilichosaidia kwa kiasi kikubwa sana kukuza na kuboresha kiwango cha Elimu nchini kwa kuwezesha miundombinu inayozunguka sekta hiyo nyeti kabisa  Ulimwenguni hivi sasa.

Katika Wilaya ya Mkalama, Mamlaka hiyo imewezesha kupatikana kwa miradi mikubwa miwili ambayo kwa namna moja au nyingine itasaidia kuinua kiwango cha udahili na ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Kitongoji cha Munguli ni eneo linapoishi kabila maarufu sana la Wahdzabe ambalo kwa miaka mingi tangu kupatikana kwa Uhuru limekuwa na mwitikio mdogo linapokuja suala la elimu hasa kutokana na kabila hilo kuishi mbali sana na mahali zinapopatikana huduma za kijamii.

Baada ya kuona changamoto hiyo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa kushirikiana na TEA wameanza Ujenzi wa bweni na bwalo la chakula la kisasa kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Munguli mradi  ambao ukikamilika  utaongeza hamasa kwa jamii hiyo kushiriki katika haki yao ya Msingi ya kupata Elimu kwa kusaidia wanafunzi hao kuondokana na changamoto ya kutembea umbali mrefu mpaka kufika shuleni na pia itawahakikishia kupata huduma bora ya chakula kwa wakati hali itakayowawezesha  kupata muda mrefu zaidi wa kukaa shuleni.

Kwa mujibu wa Mkadiriaji wa  Ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Bi. Paskazia Tibalinda Mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi milioni 184 kwa upande wa bweni na shilingi milioni 119 kwa upande wa bwalo na unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi sita kuanzia sasa.

“Zoezi la uchimbaji wa msingi limechukua muda mrefu kidogo kutokana na uwepo wa mawe kwenye udongo wa eneo hili lakini tunashukuru tumemaliza na sasa kinachofuatia na kumwaga kifusi na jamvi ambapo baada ya hapo kazi hii itaanza kwenda kwa kasi” Aliongeza Bi. Tibalinda.

Akizungumza kwa niaba ya Mamlaka ya Elimu Tanzania wakati wa ziara ya ukaguzi wa mrad huo, Meneja Uhusiano wa Mamlaka hiyo Bi. Sylvia Lupembe ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa usimamizi mzuri wa mradi huo ambapo ametoa rai ya kukamilika kwa mradi huo kwa wakati na katika ubora ulioanza nao.

“Mradi huu ni maalum kwa sababu utaisaidia jamii maalum ya Watanzania kabila la wahadzabe  lakini pia utaibadilisha jamii hii kama ambavyo wenyewe wamesema kuwa wamekaa sana porini lakini hawatoacha Mila yao ila wanahitaji kupata elimu” Aliongeza Bi. Lupembe.

Bi. Lupembe ameiomba Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kuhakikisha kuwa mradi huo unakuwa chachu ya kuchochea maendeleo ya Elimu kwa kuongeza idadi ya udahili na ufaulu wa wanafunzi wa shule hiyo ambapo alisisitiza kuwa mamlaka hiyo itaendelea kufuatilia kwa ukaribu mpaka kukamilika kwa mradi huo.

“TEA tumefarijika sana kusikia Halmashauri imeshaanza kununua vitanda kwa ajili ya wanafunzi watakaoishi kwenye bweni hili pamoja na jengo kuwa katika hatua ya awali kabisa” Alimalizia Bi. Lupembe.

Akizungumza kwa niaba ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Afisa Elimu wa Wilaya ya Mkalama kwa upande wa shule za Msingi, Chacha Kehogo alisema kuwa halmashauri imejipanga vizuri kuupokea mradi huo mara utakapokamilika ambapo mpaka sasa tayari imeshanunua vitanda 31 ambavyo vimeshafika katika shule hiyo vikisubiri kukamilika kwa bweni.

“ Kwa hiyo niwahakikisheni TEA kuwa halmashauri ya Wilaya ya Mkalama itaendelea kuunga mkono jitihada mlizozionesha ili na sisi tuoneshe tunachoweza kufanya na hata  wadau wengine wakitaka kuja wasituone tegemezi hivyo niwashukuru sana na naomba msisite kututembelea tena kwa sababu bado tuna changamoto nyingi sana katka shule zetu hasa upande wa miundombinu. ” Alimalizia Kehogo


Mbali na mradi huo TEA imekamilisha ujenzi wa nyumba bora kabisa na ya kisasa ya walimu iliyopo katika kijiji cha Isanzu yenye thamani ya shilingi milioni 148  ambapo jumla ya Walimu tisa wa shule ya Sekondari ya Isanzu wanatarajia kuanza kuishi hapo muda wowote kuanzia sasa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.