• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkalama imeadhimisha Siku ya Mtoto Afrika

Imewekwa kwenye: June 16th, 2017

Tarehe 16, juni 1976, Dunia ilishuhudia ukatili mkubwa sana pengine kuliko wowote uliowahi kufanywa dhidi ya watoto pale ambapo serikali ya Makaburu ya Afrika Kusini ilipopokea maandamano ya watoto wa shule wenye asili ya Kiafrika kwa kuwapiga risasi walipokuwa wakiandamana kupinga utaratibu wa Elimu ya kibaguzi  iliyokuwa ikitolewa wakai huo.

Ni kutokana na tukio hilo la kinyama ambalo mpaka leo bado idadi kamili ya waliouawa haijawahi kuwekwa wazi ndipo Dunia iliamua kuitumia tarehe hiyo kila Mwaka kuadhimisha sikukuu ya Mtoto wa Afrika ambapo kwa Mkoa wa Singida na Wilaya ya Mkalama maadhimisho hayo mwaka huu yamefanyika katika kijiji cha Ishenga kilichopo kata ya Kinyangiri.

Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo mwaka huu alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe: Daktari Rehema Nchimbi ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe: Mhandisi Jackson Masaka.

Katika hotuba yake, Mhe: Masaka amesema kuwa watoto ni hazina kubwa sana ya taifa, bara na dunia kwa ujumla hivyo hawana budi kutimiziwa haki zao zote za msingi.

“Haki kubwa kuliko zote ambayo kila mtoto ni lazima aipate ni Elimu na bahati nzuri Serikali yetu imeamua kuwalipia gharama za shule watoto wote kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne hivyo ni kosa kisheria kwa mzazi kumnyima mtoto haki hii ya msingi” Amesema Masaka.

Mhe: Masaka pia ametoa agizo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa kuwa halmashauri zote za Wilaya za Mkoa wa Singida zihakikishe zinatenga maeneo ya viwanja vya michezo vya watoto ili kuwaepusha watoto hao kujitengea maeneo hatarishi kama vile kwenye barabara, reli na karibu na mitambo ya umeme.

“Ni wajibu wa kila mzazi kuhakikisha anamtunza mtoto aliyemzaa na sio kumtelekeza kwa sababu kwa mujibu wa sheria za nchi yetu kuzaa ni tendo la hiyari lakini kumtunza mtoto ni lazima” Ameongeza Masaka.

Amesema kuwa ni wajibu wa kila mzazi kuhakikisha anampatia mtoto Lishe bora ili kumtengenezea mazingira mazuri ya ustawi wa akili na Mwili ambapo pia alitumia fursa hii kupiga marufuku kwa mtu yoyote kuuza mazao ya chakula katika Wilaya ya Mkalama bila kupewa kibali maalum na katibu Tawala wa Wilaya.

“Katibu Tawala wa Wilaya ndio mratibu mkuu wa suala la Ulinzi wa chakula hapa Wilayani hivyo ni lazima ajiridhishe kiasi cha akiba ya chakula uliyonayo ndipo akupe kibali cha kuuza ziada inayobakia” Amesisitiza Masaka.

Maadhimisho hayo kimkoa yalipambwa na matukio mbalimbali huku lile lililovutia hisia za watu wengi likiwa ni bunge la watoto ambapo watoto walionesha uhodari katika kuchambua kanuni mbalimbali za bunge kupitia kipindi cha maswali na majibu.

Kauli mbiu ya Siku ya Mtoto Afrika mwaka huu ni “Maendeleo Endelevu 2030: Imarisha Ulinzi na Fursa sawa kwa watoto”  ikihimiza uzingatiaji wa jukumu la Ulinzi na Usalama wa Mtoto na utoaji wa haki sawa kwa watoto wote ili kufikia malengo ya maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.