• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

SIKU TATU ZA BALOZI WA PAMBA TANZANIA WILAYANI MKALAMA KUZAA MATUNDA

Imewekwa kwenye: October 4th, 2022


Balozi wa zao la Pamba  Nchini  na Mkuu wa  Mkoa  Mstaafu  Mhe. Agrey Mwanry  leo amehitimisha ziara yake  ya kuhamasisha  kilimo cha zao  hilo kwa  siku tatu Wilayani hapa  katika   kijiji cha Ilongo na  na Igengu Kata ya  Ibaga  na kijiji cha Mpambala na Nyahaa  Kata ya Mpambala.



Akiongea na wakulima wa maeneo hayo aliendelea kuwasisitiza wakulima kufuata mbinu bora za kilimo cha pamba ambazo  zimefanyiwa  utafiti  kutoka  Taasisi ya TARI na bodi ya Pamba kushirikiana na Nchi ya Brazil  ambao ulibaini pamba ikilimwa vizuri itapelekea Mkulima  wa wilaya ya Mkalama  kupata  Kg. 2500 kwa hekari kama ilivyo kwa Nchi za Agentina , Angola , Buknafaso  pamoja na  Misri.



Katika mafunzo hayo aliwataka  wananchi kuandaa shamba mapema na kulitifua pia kuacha Ardhi  ipumue hadi majani yaanze kuota ndipo waanze kukatia na kuweka mbegu ili kuufanya udongo kupoa na kupumua.



Hata hivyo aliendelea kuwasisitiza Wakulima kuhusu matumizi ya mbolea ya Samadi katika zao hilo ambapo aliongeza kuwa mbolea ya Samadi ina uwezo wa kutunza unyevu nyevu kwa muda mrefu ambao utasaidia zao la pamba kustawi  vizuri.



‘’Mbolea ya samadi ni nzuri sana katika kilimo cha pamba kwasababu tunaweza kuipata majumbani  mwetu  ukisafisha banda la Kuku, wakinamama wakizoa majivu tayari hiyo ni mbolea  ambayo hauhitaji gharama kubwa kuipata’’ aliongeza Balozi Mwanry.



’’ Serikali imeamua kuniteua kuwa balozi wa pamba Tanzania ulishawahi kusikia  balozi wa matikiti au mchicha?  sio kwamba imelenga kujifurahisha bali kukuza uzalishaji wa pamba nakuongeza tija  katika zao hilo’’ Alisema Balozi Mwanry.



Aidha  aliongeza kuwa kwa takribani miaka mitatu sasa  uzalishaji wa zao la pamba ulishuka kutokana na mvua kuwa juu  ya wastani kwa  2020/2021  na kuwa chini ya wastani kwa mwaka 2021/2022 ambapo .



‘’Uzalishaji wa zao hili halihitaji mvua kubwa kulizalisha bali inahitaji mvua ya kawaida sana kwa asilimia 50 tu kama mnavyojua Nchi ya Misri ni jangwa lakini ndio NChi pekee inayozalisha pamba nzuri na yenye ubora wa hali ya juu’’. Alisisitiza Balozi Mwanry.



Pamoja na hayo alikutana na wakuu wa Idara na Vitengo wa halmashauri ya wilaya ya Mkalama kufanya majumuisho ya siku  tatu alizotumia katika wilaya ya Mkalama wakati akihamashisha zao hilo ambapo aliwataka Maafisa Kilimo, Maafisa Ugani pamoja na wataalamu wote kuwatembelea wakulima kila muda ili kujua maendeleo yao pamoja na changamoto zinazowakabili.



Sanjari na hayo , Mkurugenzi  Mtendaji  wa  halmashauri  ya wilaya ya Mkalama Bi. Asia Messos alimhakikishia Balozi Mwanry kuwatembelea Wakulima  pamoja na kuwashauri wananchi juu ya kilimo bora cha pamba na kusimamia kwa ukaribu ili kuwa na tija kwa zao hilo ambalo litapelekea pato la halmashauri kukua.



‘’sisi kama wilaya tutahakikisha tunawasapoti wakulima wadogo ili kuwa na tija ya uzalishaji katika zao hili’’ aliongeza  Bi. Messos.

Paia alimshukuru Balozi wa pamba Tanzania kufika  wilayani  Mkalama na kuongea na wakulima  ambapo alisema kama wilaya watahakikisha zao hilo linalimwa kwa wingi wilayani hapo.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.