• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali inatekeleza-Sanga

Imewekwa kwenye: February 7th, 2018

“Jana Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama imepokea fedha kwa ajili ya kumalizia miundombinu yote ya Zahanati za Kidarafa, Milade na Nduguti hivyo muda si mrefu tutafungua Zahanati hizo na Wananchi wa maeneo hayo wataanza kupata huduma zote stahiki za kiafya”

Hiyo ni kauli iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Mhandisi Godfrey Sanga alipokuwa katika kijiji cha Kinyambuli kukagua ujenzi wa Kituo bora na cha Kisasa cha Afya Unaoendelea kijijini hapo.

Mradi huo unaogharimu kiasi cha Shilingi milioni 700 unatarajiwa kukamilika ifikapo Mwezi Aprili Mwaka huu ambapo jumla ya Shilingi milioni 400 zilipokelewa na Halmashauri ya Wilaya na Kuhamishiwa katika akaunti ya Serikali ya Kijiji hicho ili kurahisisha utekelezaji wa mradi huo kwa wakati.

“Shilingi Milioni 300 zilizobaki zitatumika kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa ambapo tayari tumeshazielekeza Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ili pindi tu Kituo kitakapokamilika huduma ianze mara moja” Alisisitiza Sanga.

Sanga alibainisha faida kadhaa ambazo wananchi wa Wilaya ya Mkalama kwa ujumla watanufaika nazo baada ya kukamilika kwa kituo hicho ikiwa ni pamoja na kusogezewa karibu huduma muhimu na za lazima ikiwemo ile ya Kuhifadhi Maiti na Kufanya Upasuaji ambapo Wananchi wa Mkalama wanalazimika kwenda mpaka hospitali ya Hydorm kwa ajili ya kupata huduma hizo.

“Lakini pia ninapenda kuwajulisha kuwa katika mwaka ujao wa Fedha Halmashauri inakusudia kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambapo tayari eneo la kujenga hospitali hiyo limeshatengwa na kinachosubiriwa ni Fedha tu kwa ajili ya kuanza Utekelezaji wa Ujenzi wa Hospitali hiyo” Aliongezea Sanga.

Mpaka kufika mwezi Juni mwaka huu Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama inatarajiwa kupiga hatua kubwa katika sekta ya Afya baada ya kukamilika kwa wodi ya wazazi ya Zahanati ya Nduguti, Vifaa tiba na miundombinu yote katika zahanati ya Milade na Kidarafa na Ujenzi wa Majengo ya Chumba cha Upasuaji, wodi ya Wazazi, Maabara ya Kisasa, Chumba cha Kuhifadhia Maiti na Nyumba bora ya Watumishi wa kituo hicho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.