• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI IMEJIPANGA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Imewekwa kwenye: February 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba amesema kuwa Serikali imejipanga kutatua kero za Wananchi kwenye masuala ya Miundombinu ya barabara , maji , Afya , umeme  na Elimu ili kuhakikisha mwananchi anapata huduma hizo ipasavyo.

Mhe. Serukamba ameyasema hayo leo Februari 21, 2023 katika Kijiji cha Gumanga , Kata ya Gumanga Wilaya ya Mkalama  wakati wa muendelezo wa ziara zake za kusikiliza na kutatua kero za Wananchi .


Mhe. Serukamba aliongeza kuwa kero zote walizoziwasilisha mbele yake zitatatuliwa na kushughulikiwa  kwa wakati kabisa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

‘’Niwapongeze wananchi wa Kijiji cha Gumanga kujitokeza kwa wingi na kuja kuwasilisha changamoto zenu, nimefurahi kuona mna ari ya kuuliza maswali  na kero zote mlizowasilisha ni za kutaka maendeleo, ninawahakikishia yote nimeyachukua na nitayafanyia kazi ‘’ Aliongeza Mhe. Serukamba


Kufuatia kero za miundombinu ya barabara Mhe. Serukamba  alimuagiza Mhandisi wa Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini ( TARURA) kutembelea barabara ya Kinankamba , Ikungu mpaka Mkiko na ile ya njia panda ya Ikungu- Kinandili inayoenda Miganga ili kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo wanaunganishwa na mtandao wa barabara hizo ili waweze kupitisha mazao yao na kufanya shughuli mbalimbali za kujiongezea kipato na kukuza uchumi.


Katika hatua nyingine Mhe. Serukamba amewataka watendaji wa Vijiji na Kata kuhakikisha wanatumia nafasi zao kutatua kero za wananchi na kutenda haki  ikiwa ni pamoja na kuacha kubagua wananchi kutokana na  itikadi zao za dini au Chama.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali amesema kuwa kwa kushirikiana na vingozi wake watahakikisha wanatatua na kushughulikia kero zote za wananchi Wilayani Mkalama ikiambatana na ripoti na namna walivyotatua changamoto .


Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkalama Bw. Lameck Itungi amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Singida kuanzisha ziara ya kutembelea kila wilaya kwaajili ya kutatua changamoto hii inaonyesha Ilani ya Chama cha Mapinduzi inatekelezwa vizuri nakuahidi kuwa uongozi wa Chama Wilaya ya Mkalama wapo bega kwa bega kuunga mkono juhudi hizo.


Akiongea kwa niaba ya Wananchi ,  Diwani wa Kata ya Gumanga na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. James Mkwega amesema wananchi wa Kata hiyo wamefurahi kuona Mkuu wa Mkoa anafika kwenye maeneo yao kusikiliza na kutatua changamoto zao ambapo aliahidi ushirikiano mkubwa katika kuunga mkono juhudi hizo ambapo pia aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi wanaposikia mikutano ya namna hiyo ili kero zao zisikilizwe na kupatiwa ufumbuzi

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.