• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali imejipanga kikamilifu kutatua kero za Wananchi

Imewekwa kwenye: July 17th, 2022

Waziri  Mkuu wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa   Kassim  Majaliwa  amesema serikali imejipanga  kutatua kero zote za wananchi ili kuhakikisha kila mwananchi anapata  huduma  bora  huku akiwataka watumishi  kila mmoja kwa nafasi yake kuwatumikia wananchi kwa kuwatembelea   kwenye maeneo yao  kusikiliza na kutatua kero zao.


Amesema hayo leo wakati wa ziara yake ya Kikazi aliyoifanya July 17 2022 wilayani Mkalama ambapo katika ziara hiyo  alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi  wa   daraja la mawe lilijengwa katika barabara ya Iguguno- Kikhonda- Kinampundu  lenye urefu wa mita 30 na upana wa mita 7 katika  kijiji Cha Lukomo  lenye thamani ya sh Mill 102 pamoja na  kuzindua ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Mkalama iliogharimu kiasi cha sh Bill 1.33.


Aidha  Mheshimiwa  Majaliwa  aliongea na Wananchi wa Wilaya ya  Mkalama na kusema kuwa  Serikali  ya  awamu ya sita imekusudia  kuleta maendeleo kwa wananchi  ndio maana imekua ikitoa fedha nyingi  kwaajili ya kutekeleza  miradi ya maendeleo na kuwataka kuunga mkono juhudi hizo kwa kufanya kazi kwa bidii.


Hata hivyo  Mheshimiwa Majaliwa  aliwapongeza  Wahandisi  wa wakala wa Barabara  Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA)  kwa ujenzi wa daraja zuri na lenye ubora kwakutumia teknolojia rahisi ya  mawe na kusema  daraja hilo litakua mkombozi  kwa wananchi wa kijiji cha  Lukomo na wilaya kwa ujumla.


Alisema ipo haja ya wahandisi  wengine kuiga taaluma hiyo ya mawe kwa kila Mkoa  kwakua kila Mkoa una mawe mengi jambo ambalo litaweza kupunguza gharama za ujenzi  na kuokoa fedha  nyingi za serikali katika ujenzi huo.


Aidha Mheshimiwa Majaliwa aliwapongeza wakala wa Majengo Tanzania TBA  kwa kukamilisha ujenzi wa   Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa asilimia  100 na kuridhishwa  na ubora wa Ofisi hiyo huku akisema  kukamilika kwa ofisi hiyo utarahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi  wilayani hapo.


‘’wahandisi wetu wa TBA Tanzania sasa ninaweza kufungua,  siwezi  kufungua bila kukagua ,ndio sababu niliingia huko ndani kuona  kama nyumba inatosha  na ina viwango? na nyie mmeona viwangoee  kwahiyo nimeridhika na viwango’’alisema Mheshimiwa Majaliwa.


Naibu waziri  wa Ofisi ya Rais Tamisemi  Festo Ndungange  alisema  serikali imetoa Bill 2.6 katika sekta ya Afya wilayani Mkalama  kwaajili ya kujenga vituo vya afya,  vifaa tiba , huduma za upasuaji huku akisema serikali imetoa  Bill. 2.6 kwaajili ya kuboresha miundo mbinu ya elimu  kwakukamilisha madarasa ya shule za msingi  na Sekondari.


Pamoja na hayo Mh. Ndungange alisema serikali imeongeza bajeti ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini Tarura kutoka mill 600 hadi bill. 2 lengo ni kuunganisha barabara kupitika kwa urahisi ili kuchochea maendeleo ya wilaya,  hivyo kuwataka wananchi kuunga mkono juhudi za serikali kwa kutunza miundombinu hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.