• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SERUKAMBA AZINDUA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WILAYANI MKALAMA

Imewekwa kwenye: January 14th, 2023

Rc Serukamba akipanda mti katika kampeni aliyoizindua Leo January 14 2023 wilayani Mkalama


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba amesema Serikali ya Mkoa wa Singida imejipanga kupanda Miti milioni tatu ili kurudisha uoto wa asili na kuufanya  Mkoa kuwa wa kijani.


Amesema hayo mapema leo wakati akizindua zoezi la upandaji Miti Wilayani Mkalama iliyohusisha maeneo ya Njia panda ,  Barabara kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, maeneo ya chanzo cha maji Nduguti pamoja na Hospitali ya Wilaya.


Aidha,  Mhe. Serukamba alitumia fursa hiyo kuongea na  Viongozi pamoja na Wananchi wa Wilaya ya Mkalama na kuwapongeza kuendeleza zoezi la upandaji miti ambapo aliwataka kila mtu kuwa balozi mzuri wa mazingira na kuagiza kila mwananchi kupanda Miti minne kila nyumba kuhakikisha Mkalama inakuwa ya kijani ili kukabiliana na mabadiliko tabia ya nchi.


‘’Mkoa wa Singida tumejipanga kupanda Miti ya kutosha  ipatayo milioni tatu na ili tufikie lengo hilo ni lazima kila Mwananchi apande Miti minne  kwa kila kaya, tukipanda Miti Mkalama itavutia na kupendeza na kila mtu atavutiwa kuja kukaa Mkalama’’ Aliongeza Mhe. Serukamba.


Pamoja na hayo Mhe. Serukamba aliwashukuru Wananchi wa Wilaya ya Mkalama kujitokeza kwa wingi kupanda Miti, hivyo kuwataka kila mmoja kutunza na kuilinda Miti iliyopandwa tarehe 14/01/2023 ili iweze kuwaletea hewa safi pamoja kurejesha uoto wa asili kwa faida ya vizazi vya baadae.


Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkalama, Bi. Elizabeth Rwegasira  aliwapongeza Watumishi wote wa Wilaya pamoja na Wananchi wa  Nduguti , Maziliga na vijiji jirani kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kupanda Miti na kusisitiza kuwa zoezi hili ni  endelevu na lilianza toka siku ya Uhuru na  leo  Miti Mia tano thelathini  imepandwa na kuahidi  usimamizi mzuri ili kuunga mkono juhudi za Serikali  za kurudisha uoto wa asili kila sehemu.


Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkalama, Bw. Lameck Itungi pamoja na Mwenyekiti  wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. James Mkwega wamesema zoezi hili ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi na watahakikisha Wilaya inasimamia zoezi hili kikamilifu pamoja na kuwepo kwa Sheria zinazosimamia utunzaji wa Mazingira na kuweka utaratibu kila Kijiji kuwa na hifadhi ya Msitu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.