• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SERUKAMBA AZINDUA MRADI WA BIL. 34

Imewekwa kwenye: June 14th, 2023


RC SERUKAMBA AZINDUA MRADI WA UMWAGILIAJI WA BIL.34/-SKIMU YA MSINGI WILAYANI MKALAMA


MKUU wa Mkoa wa Singida,Mhe. Peter Serukamba, leo (Juni 14, 2023) amezindua Mradi wa Skimu ya umwagiliaji utakaogharimu zaidi ya  Shilingi Bilioni 34. 176 utakaotekelezwa katika Kijiji cha Msingi, Kata ya Msingi Wilayani Mkalama mkoani Singida.


Akizungumza wakati wa makabidhiano ya mradi huo ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 18, amesema Mradi wa Skimu ya Msingi utakuwa na jumla ya eneo la hekta 2,000.

Mhe Serukamba amesema mradi huu utakapokamilika utawanufaisha wakazi 12,000 kutoka Vijiji vinne vya Ishinsi, Ndurumo, Msingi na Kidi vilivyopo Kata ya Msingi tarafa ya Kinyangiri ambao watalima mazao ya mpunga,mahindi na mbogamboga Kwa misimu miwili hadi mitatu kwa mwaka.


Ameongeza kwakusema kuwa  shughuli kuu zitakazofanyika katika shughuli ya ujenzi wa mradi ni ujenzi wa bwawa lenye ujazo wa Lita 1,875,000,ujenzi a mifereji ya umwagiliaji yenye kilometa 19.12, uchimbaji wa mifereji ya matupio yenye urefu wa kilo mita 42.539, uchimbaji wa mifereji ya kuingiza Maji mashamba yenye urefu wa jumla ya kilometa 34.778.


Shughuli nyingine zitakazofanyika ni ujenzi wa barabara za mashamba zenye urefu wa kilomita 36.1, kusawazisha ekari 2,000 za mashamba,ujenzi wa kilomita nane za barabara na makaravati sita kuelekea ndani ya mradi na ujenzi wa vigawa Maji 14,vipunguza mwendo,viumbo angalizi 90,vipitisha maji 90,makaravati 14 pamoja na vivuko nane.

Mhe .Serukamba amesema Ili mkandarasi aweze  kuendelea na kazi za ujenzi bila kukwama Tume ya Umwagiliaji ihakikishe inamlipa mkandarasi kila anapokamilisha hatua mojawapo ya ujenzi.


Akizungumza na wananchi wa vijiji vitakavyonufaika na mradi huo katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la mradi aliwataka wananchi kutouza ardhi kwani lengo la Serikali ni kutaka wenyeji wanufaike na mradi huo.

Mhe. Serukamba aliwaondoa hofu wananchi kwamba watanyang'anywa ardhi kwamba hizo ni propaganda hakuna atakayenyang'anywa na kuagiza wenyeviti wa vijiji kusimamia kuhakikisha kila mwananchi anapata eneo la kulima.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhe.Moses Machali, ametuamia fursa hiyo kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha  za ujenzi wa mradi huu  kwani utasaidia kuinua uchumi wa wilaya ya Mkalama

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mhe. James  Mkwega, amesema fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan katika mradi huu ni nyingi hivyo watahakikisha wanautunza mradi ili wanufaike na kubadili maisha ya Wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.