• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC SERUKAMBA AWATAKA VIONGOZI KUTATUA MIGOGORO YA WANANCHI

Imewekwa kwenye: January 18th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba ameutaka uongozi wa Wilaya ya Mkalama kuweka ratiba ya kutembelea Wananchi Vijijini kusikiliza kero zao pamoja na kutatua migogoro ya Ardhi ambayo inaoneka ni tatizo sugu Wilayani hapa.


Amesema hayo mapema leo January 18, 2023 wakati akisikiliza kero za wananchi Wilayani hapa ambapo pia aliagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kupitia Maafisa Ardhi kusimamia kurudisha Ardhi ya Edina Philipo Mkumbo na Melisiana Nelson Mnoma ambao wana mgogoro na Serikali ya Kijiji cha Yulansoni.


‘’mimi ni muumini wa haki na muumini wa kutatua kero za Wananchi hivyo ninawataka  Wakuu wa Idara na Vitengo msikae ofisini wekeni ‘program’ ya kwenda Vijiji msikilize na kutatua changamoto za Wananchi na sio kuwaachia Serikali ya Kijiji, haiwezekani Serikali ya Kijiji ikabeba hatima ya Wananchi wa Mkalama.’’ Aliongeza Mhe. Serukamba.


Aidha, Mhe. Serukamba aliwataka Maafisa Ardhi kwenda kwa wananchi kupima Ardhi yao pamoja na kuwapatia Hati Miliki ili kuondoa migogoro inayotokana na Ardhi pamoja na kuwataka kutafuta jengo kwa ajili ya Baraza la Ardhi Wilaya ili wananchi waweze kusikilizwa mashauri yao Wilayani hapa  na kuacha kufuata huduma hiyo Wilayani Iramba.


‘’Niwaombe Maafisa Ardhi kutafuta jengo kwa ajili ya Baraza la Ardhi Wilaya kama Mwenyekiti wa Baraza yupo mnasubiri nini kutoa huduma, tumieni hata Ukumbi wa Halmashauri siku ya Baraza ili wananchi wote wapate huduma Wilayani Mkalama kwani wengi hawana uwezo wa kwenda Iramba’’ alisisitiza Mhe. Serukamba.


Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Katibu Tawala Wilaya Bi. Elizabeth Rwegasira amemshukuru Mkuu wa Mkoa kufanya ziara Wilayani hapa pamoja na kusikiliza kero, hivyo kuahidi kuwa watatekeleza maelekezo yote aliyoyatoa pamoja na kuwasilisha ripoti ya namna walivyoshughulikia na kutatua kero za Wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.