• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

NIWAPONGEZE TRA KUVUKA LENGO LA UKUSANYAJI WA MAPATO

Imewekwa kwenye: May 31st, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Mhe. Mosses Machali ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA) Wilaya ya Mkalama  kwa kuongeza usajili wa Wafanyabiashara wapya wapatao 477 pamoja na kuvuka lengo la ukusanyaji wa Mapato kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo walikusudia kukusanya  Milioni 250 lakini wakakusanya Milioni 277 na mwaka 2022/2023 kukusanya Milioni 700 hadi kufikia leo Mei 31 2023 wamekusanya Milioni 611.


Ametoa pongezi hizo katika kikao cha Kamati ya Ushauri wa Kodi Wilaya ya Mkalama yenye lengo la kupitia utendaji wa kazi wa Mamlaka ya Mapato Wilaya inayojumuisha Wafanyabiashara mbalimbali wanaochangia na kutoa dira juu ya hali ya biashara  na ukusanyaji mapato Wilayani hapa.

‘’Niwapongeze ‘TRA’ kwa ukusanyaji wa mapato na kuvuka lengo mlilojiwekea kutoka mwaka 2021/2022 na kwa mwaka 2022/2023 ambapo hadi sasa mmekusanya Milioni 611 na hapa Meneja katuambia hadi kufika june 30 mtakuwa mmevuka lengo’’ Aliongeza Mhe. Machali.


Mhe. Machali amesisitiza ushirikiano baina ya Mamlaka ya Mapato, TARURA, Halmashauri ya Wilaya pamoja na Taasisi zote Wilayani hapa ili kuongeza ukusanyaji wa mapato Wilayani pamoja na kuitaka Kamati kuhakikisha kila mmoja kwa nafasi yake anasimamia suala hilo kikamilifu kwa maendeleo ya ya wananchi.


Awali akiwasilisha taarifa Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Wilaya ya Mkalama CPA. Iddi Omary  amesema kuwa kwa kushirikiana na Halmashauri na TARURA wanatarajia kuongeza ukusanyaji na kuvuka lengo walilojiwekea la kukusanya Sh. Milioni 700 kwa 2022/2023 huku akiongeza kwa mwaka wa fedha 2023/2024 wamejipanga kukusanya sh 1.5 Bilioni.


Pamoja na hayo CPA Omary aliongeza kwakusema TRA Wilaya pamoja na kutoa mafunzo ya kuwajengeza uwezo Kamati pamoja na kuendelea kutumia mashine za Kielekitroniki (EFD) katika kutoa risiti ili wananchi waendelee kufurahia huduma iliyobora Zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.