• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ni wajibu wa kila mtanzania kuulinda utamaduni wetu-Mlawi

Imewekwa kwenye: October 7th, 2018

Mkoa wa Singida kupitia Wilaya ya Mkalama na mkoa wa Manyara kupitia wilaya ya Mbulu leo wameadhimisha tamasha la pamoja la utamaduni wa makabila makuu yaliyopo kwenye mikoa hiyo tukio lililofanyika katika kijiji cha Hydorm.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa utamaduni na Michezo Bi. Suzan Mlawi ambaye alizipongeza wilaya hizo kwa kufanikisha maadhimisho ya tamasha hilo huku akisisitiza kuwa suala la kudumisha mila na utamaduni wa watanzania ni jukumu la kila mwananchi.

“Mwalimu Nyerere aliwahi kusema Taifa lisilo na utamaduni ni sawa na taifa lililokufa hivyo ni lazima kila mmoja wetu aenzi na kudumisha mila na desturi zetu kwani ndio kitambulisho chetu hata tunapokuwa nje ya nchi yetu” Alisisitiza Bi. Mlawi.

Bi Mlawi aliongeza kuwa maadhimisho hayo ni ishara kubwa inayoonesha ushirikiano wa dhati uliopo baina ya Wilaya ya Mkalama na Mbulu ambapo aliwasihi viongozi wa pande hizo mbili kuendeleza na kudumisha umoja huo huku wakiendelea kuenzi mila na desturi za Mtanzania.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka aliipongeza kamati ya maandalizi ya tamasha hilo na kuwataka wananchi wote wa Wilaya ya Mkalama kuhakikisha wanajitokeza kwenye tamasha hilo ambalo litafanyika kila mwaka.

“Kuhudhuria tamasha hili ni utalii tosha kabisa na mtu anaweza kuja na familia yake kwa ajili ya mapumziko hivyo nawasihi wananchi wa Mkalama na maeneo mengine ya jirani wafike kushuhudia tukio hili la asili kabisa” Alisisitiza Mhe. Masaka.

Tamasha hilo lilipambwa na burudani mbalimbali za asili kutoka makabila ya Wagogo, Wasukuma, Wangoni, Wahadzabe, Wanyiramba, Wanyisanzu,  Wairaqi, Wamasai na Wadatoga huku kivutio kikubwa kikiwa ni vipaji vilivyooneshwa na mbunge wa jimbo la Mbulu vijijini  Mhe. Flatei Massay na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka ambao walionesha ustadi mkubwa katika kucheza ngoma na nyimbo za asili.

Mbali na ngoma na nyimbo za asili kutoka katika makabila tofauti, tamasha hilo lilijumuisha pia maonesho ya vitu mbalimbali vya asili, wanyamapori kama vile Simba, Chui, Mamba na kobe mwenye umri wa miaka 200 na utamaduni wa kabila la wadatoga.

Kijiji cha Hydorm kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Mkalama na Mbulu kwa sasa kinatambulika kama kitovu cha Afrika kutokana na kujumuisha makundi makuu manne ya jamii za bara la Afrika ambao ni Wanyiramba na Wanyisanzu (Wabantu), Wadatoga (Wanailo), Wahadzabe (Wakwesa) na Wairaqi (Wakushi).

Makundi hayo pamoja na kuishi pamoja kama ndugu katika kijijichi hicho wanatofautiana katika lugha, historia, utamaduni na mgao wa utumiaji wa rasilimali.

Miongoni mwa wadhamini wakubwa wa tamasha hilo kwa mwaka huu  ni pamoja na serikali ya Norway chini ya kitengo cha Utamaduni kinachojulikana kama 4CCP (4 Corners Cultural Programs), Mbuga ya wanyama ya Ngorongoro, Kampuni ya Yara, Shirika la bima ya afya la MHI na  benki ya CRDB.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.