• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ni marufuku Waalimu kupokea Michango shuleni-Nchimbi

Imewekwa kwenye: January 26th, 2018


“Kuanzia sasa jukumu la kukusanya na kusimamia michango ya aina yoyote ile shuleni lifanywe na wazazi wa wanafunzi hao kupitia bodi za shule badala ya walimu na kuanzia sasa mwalimu haruhusiwi kumrudisha nyumbani mwanafunzi mwenye upungufu wa mahitaji ya shule na badala yake amshirikishe mzazi juu ya umuhimu wa mahitaji hayo ili mzazi kwa hiyari yake aweze kutimiza majukumu yake ya msingi kwa mwanae akiwa shuleni”




Hayo ni maneno yaliyozungumzwa na  Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Daktari Rehema Nchimbi alipokuwa katika ziara yake Kijiji cha Munguli mapema jana ambapo alifika kwa ajili ya kukagua mradi mkubwa wa Maji na kuzindua darasa la kisasa la shule ya Msingi Munguli na Ofisi ya Walimu miradi yote ikiwa imewezeshwa na Mashirika yasiyo ya kiserikali kutoka nchini Norway yanayojulikana kama ‘Norwegian Church Aid’ (NCA) na ‘4 corners Cultural Program’ (4CCP).




Mhe. Nchimbi ameyapongeza mashirika hayo kwa kuwezesha ujenzi wa miradi mikubwa katika kijiji cha Munguli ambapo aliongeza kuwa undugu huo kati ya Wilaya ya Mkalama na mashirika hayo unapaswa kuenziwa kwa njia ya utunzaji bora wa miradi hiyo ili kuwapa nguvu wafadhili hao kuendelea kuboresha miundombinu mingine iliyopo Wilayani hapa.




“Ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwenu na mimi huwa napenda kusema kuwa kushukuru ni kuomba tena hivyo ninawaomba kama ilivyowapendeza kwa upande wa Munguli Magharibi, muiangalie Munguli Mashariki kwa jicho hilo hilo kwani nao wanahitaji sana miradi mliyoiweka hapa kwa wenzao” Aliongeza Mhe. Nchimbi.

Suala la upandaji wa Miti ya Korosho na matumizi mazuri ya Fedha zinazotolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ni moja ya mambo yaliyosisitizwa na Mhe. Nchimbi katika hotuba yake kijijini hapo ambapo aliagiza wakuu wa shule zote za Msingi na Sekondari kuhakikisha wanapanda korosho katika mashamba ya shule zao na walengwa wote wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii wanatumia fedha hizo kujikwamua kiuchumi badala ya kuzitumia kwenye ulevi na anasa nyingine.



Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Mhandisi Jackson Masaka  aliyashukuru Mashirika ya NCA na 4CCP kwa kuwezesha miradi hiyo mikubwa Wilayani kwake ambapo aliwaagiza wananchi wa Kijiji hicho kuhakikisha hawafanyi shughuli za kiuchumi katika maeneo yaliyo karibu na mradi wa Maji ili kuweza kuulinda mradi huo.



Kwa upande wake Afisa Miradi wa Mashirika ya NCA na 4CCP Nelson Faustineamewashukuru viongozi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa ushirikiano Mkubwa waliouonesha katika kipindi chote cha Ujenzi wa Miradi hiyo jambo ambalo alikiri kutolipata kwa kiwango hicho  katika maeneo mengine yote waliyotekeleza miradi yao.



“Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wametuonesha ushirikiano mkubwa sana na ilifikia hatua tulikuwa tunawapigia simu muda wowote tunaaohitaji msaada wao na wao hawakusita kutusaidia” Alisisitiza Faustine.


Mashirika ya NCA na 4CCP yametekeleza miradi hiyo  kwa kushirikiana na Kanisa la Kilutheri la Hydom lililopo Wilayani Mbulu Mkoani Manyara.














Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.