• Wasiliana nasi
    • Maswali
    • Barua Pepe
    • Malalamiko
Mkalama District Council
Mkalama District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo
      • Usimamizi wa Mazingira
      • Biashara na Fedha
      • Afya
      • Ardhi na Mipango ya Mji
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Miundombinu
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Kisheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi, Ugavi & Vifaa
      • TASAF
      • Biashara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Kilimo
    • Mfumo wa Taarifa za Shule Tanzania
    • Uvuvi
    • Sekta ya Huduma
    • Ardhi iliyotengwa kwaajili ya Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Utawala na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
      • mwongozo kutoka Tamisemi
      • uongozi ngazi ya vijiji
      • vibali vya ujenzi
      • mfumo wa anwani za makazi
    • Ripoti
      • Taarifa ya CAG 2018
    • Sheria
      • sheria ya fedha
    • mkataba
    • Fomu za Maombi kwa Wateja
      • Leseni ya biashara
      • maombi ya kiwanja
      • leseni za vileo
    • Sera
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
      • Pongezi
      • Matokeo ya Uchaguzi Kinampundu
      • KURUDISHWA KAZINI
      • Juma la elimu
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

NDANI YA SIKU 10 KILA NYUMBA IWE NA CHOO IMARA NA CHAKUDUMU 'DC MACHALI '

Imewekwa kwenye: November 8th, 2023
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali leo Novemba, 08,2023 amewataka wenyeviti wa Vijiji, Watendaji wa Vijiji, Watendaji wa Kata pamoja na Tarafa kuhakikisha kaya zote Wilayani Mkalama zinakuwa na vyoo na kutoa siku kumi kwa kwaya ambazo hazina vyoo kujenga na kuwaagiza kuwachukulia hatua kali za kisheria watakao kiuka agizo hilo ili kukabiliana na ugonjwa wa mlipuko wa homa ya kutapika na kuharisha[Kipindupindu].


Ametoa maagizo hayo mapema leo katika ukumbi wa Sheketela uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ambao pia ulihususisha viongozi wa taasisi mbalimbali  na dini ambao aliwata kila mmoja kwa nafasi yake kusimamia suala hili ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo.


Mhe. Machali amesema kuwa ugonjwa wa kipindupindu unasababishwa na uchafu wa mazingira ikiwepo kaya nyingi wilayani hapa kukosa vyoo bora hivyo kuwaagiza Watendaji hao kuanzia kesho novemba, 09, 2023 kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo yao ili wananchi  wapate elimu ya usafi wa mazingira pamoja na kuwa na vyoo bora.


‘’Maelekezo yangu ni kwamba nendeni kwenye maeneo yenu wewe  Mwenyekiti wa kijiji ,mtendaji wa kijiji, Kata mkahakikishe ndani ya siku 10 kila kaya inakuwa na choo bora natoa maelekezo  kuwachukulia hatua kali za kisheria watakao puuza agizo hilo’’ Alisisitiza Mhe.Machali.


 Pamoja na hayo aliwataka viongozi wa dini wanapokuwa kwenye nyumba zao za ibada kutoa elimu kwa waumini wao kuhusu hatari kuwepo kwa maambukizi ya ugonjwa huu hatari wa mlipuko na kuwataka kuchukua tahadhari zote za kiafya katika kuzuia maambukizi hayo kuenea katika maeneo mengine.


Aidha ameagiza kuwepo kwa vyoo katika maeneo yote ya taasisi za umma,  mashirika ya dini, soko, shuleni, stendi ya mabasi , nyumba za ibada  na kwenye mikusanyiko kuwepo vifaa vya kunawia mikono ikiwepo sabuni na vitakasa mikono ambapo amewataka wananchi kuacha kusalimiana kwakutumia mikono ili kuzuia maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.


Sanjari na hayo amemuagiza Meneja wa Wakala wa maji na usafi wa mazingira Wilaya ya Mkalama( RUWASA)  kuchukua sampuli za Maji  pamoja na kutibu visima virefu na vifupi ndani ya Wilaya ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa kutapika na kuharisha ( KIPINDUPINDU).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI KUANZIA TAREHE 09-10-2024 HADI 14-10-2024 October 03, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA MKALAMA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

    April 24, 2025
  • WANAWAKE MKALAMA WAHIMIZWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

    March 06, 2025
  • DC MACHALI ATOA WITO WATU WA AFYA MKALAMA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    February 19, 2025
  • SEMINA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI MKALAMA

    February 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Taarifa ya fainali kati ya Kisuluiga na Nkungi
Video Zaidi

Viungo Haraka

  • eMrejesho -Tuma Malalamiko, Maoni au Pongezi
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja

Viungo vinavyohusiana

  • Utumishi
  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKALAMA, 18 MASAKA RD, 43582

    Anuani ya Posta: P.o. Box 1007

    Simu ya Mezani: 026-2964005

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@mkalamadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 Mkalama DC . All rights reserved.